Tuesday, September 25, 2012

Video shots


Rule 1: The most important rule when videotaping people is to always compose your shot so that the subject is cut off in between joints. Even if you are videotaping Lego characters this rule still applies! Don't cut your subjetc at the knee, neck, elbow or waist. Try to think about this when you plan the shots in your storyboard.
Rule 2: Always shoot one scene from one angle and then move the camera or change the angle for the next shot. If you don't do this you will get a "jump cut." The example here shows a jump cut and and then a second take of the same scene without a jump cut.
ECU - Extreme CloseupECU - Extreme Closeup
The extreme close up is used to reveal very small details in the scene. It might be used to reveal horror in a subject (extreme close up of the subject's mouth as she/he screams). It might also be used in a mystery to show some detail that the detective picks up on or to show some small clue.
CU - Close UpCU - Close Up
The close up shot is used to reveal detail. If you are shooting just the head and shoulders of a subject this is a close up.
Head and ShouldersHead and Shoulders
The head and shoulders shot is used in news broadcasts. If you think about the television news you will realize that this shot reveals enough detail to see the subject's lips move and the expression on her/his face.
Bust ShotBust Shot
This shot shows your subject from above the knees to above the head. It is often used when the subject of the shot is doing something that requires the audience to see some detail.
MS - Medium ShotMS - Medium Shot
The medium shot is from just below the waist to above the head. There is more headroom than in the bust shot. This show is used if the person is animated with their hand movements, etc.

MLS - Medium Long ShotMLS - Medium Long Shot
Remember in this shot to not cut ther person off at the knees. With this shot, you can still see expression on the persons face, while getting more information from what is going on around the person.
LS - Long ShotLS - Long Shot
This shot is useful for someone that is walking or moving.
ELS - Extra Long ShotELS - Extra Long Shot
Also known as the Establish shot, this gives the viewer some perspective as to where the subject is. This is very important if the subject is moving to new locations or times. It lets the viewer know where the video is taking place.
2 Shot 2 Shot
Two-shots are composed when two people are in the scene and their interaction is important. A two-shot is a good way to introduce a conversation. From the introduction you might cut to an over the shoulder shot of one person talking or a close-up of the other person reacting to what is being said.
OS - Over Shoulder OS - Over Shoulder
The over the shoulder shot reveals one subject as seen from over the shoulder of another subject. It simulates a view of the subject as seen from the second person's eyes. This shot is often used in conversations between two people where the dirtector wants to focus on the person speaking. Usually these shots are head shots (close ups of the speaker).

Camera Techniques




Zoom
Description: View of subject changes from tight to wide or wide to tight using the zoom control on the lens. The camera does not move. Pg. 7
Purposes: Change focus of attention from broad view to detail of subject or vice versa, keep size of moving subject the same in frame, reveal surroundings of subject (zoom out). Provides sense of magnifying subject without getting physically closer (zoom in).
Video Clip
Play 56k Modem.Play DSL.
Follow Action
Description: Camera follows subject as they move. May involve panning, tilting, and zooming.
Purposes: Keep subject in frame, add energy and movement to scene.

Let in/out
Description: Camera is stationary and subject enters or leaves frame.
Purposes: Allow subject to enter or leave scene, a transition between scenes or subjects. Let in can establish a setting and then bring attention to subject walking into setting. Let out can be used to end a scene.

Let in & Follow
Description: Subject enters camera frame and then camera follows moving subject.
Purposes: Establish a scene and then follow action, change attention from one subject to another, pickup pace of scene, transition between subjects.

Shift Attention
Description: Uses a pan, tilt or combination to change the main subject of a shot from one element to another.
Purposes: Shift attention from one element in the frame to another, show physical relationship between subject elements, follow action by changing framing when main action changes between subject elements or show secondary activities happening while main action occurs.
Video Clip
Play 56k Modem.Play DSL.

Camera Shots




Wide Shot
Description:Shows whole body or space.
Purposes: Establish scene or setting, allow room for action.
Wide Shot
Wide Shot

Medium Wide Shot

Description
: Shows most of body or space.
Purposes: Allows room for movement and other subjects to enter frame.
Medium Wide Shot

Medium Shot

Description: Shows subject from waist up.
Purposes: Allows connection with subject while providing room for gestures. Most frequently used shot.
Medium Shot

Bust Shot
Description: Shows subject from mid-chest area up.
Purposes: Provides intimate view of subject, focuses attention on face.
Bust Shot

Medium Close Up
Description: Shows part of subject.
Purposes: Focuses attention to details.
Medium Close Up

Close Up
Description: Shows enlarged view of part of subject.
Purposes: Draws attention to details and adds emotion.
Close Up

camera movement


Pan
Description: Shows what's to the left or right of the screen. Pg. 2.
Purposes: Reveal setting, sweep across subject wider than screen, show relationship between two subjects.
Video Clip
Play 56k Modem.Play DSL.
Tilt
Description: Shows what's above or below the screen. Pg. 3.
Purposes: Reveal parts of vertical subject, useful for showing tall objects, show relationship between parts of a subject, can add suspense or surprise.
Video Clip
Play 56k Modem.Play DSL.
Truck
Description: Camera physically moves to left or right around subject.
Purposes: Reveal another side of subject, add dimension, show physical relationship between objects or subjects.

Dolly
Description: Camera physically moves toward or away from subject. Pg. 4.
Purposes: Change focus of attention from broad view to detail of subject or vice versa. Provides sense of physically moving closer or farther from subject.
Video Clip
Play 56k Modem.Play DSL.

Shot Types

amera Work : Shots


There is a convention in the video, film and television industries which assigns names and guidelines to common types of shots, framing and picture composition. The list below briefly describes the most common shot types (click the images for more details).
Notes:
  • The exact terminology varies between production environments but the basic principles are the same.
  • Shots are usually described in relation to a particular subject. In most of the examples below, the subject is the boy.
  • See below for more information and related tutorials.
Extreme Wide Shot
EWS (Extreme Wide Shot)

The view is so far from the subject that he isn't even visible. Often used as an establishing shot.
Very Wide Shot
VWS (Very Wide Shot)

The subject is visible (barely), but the emphasis is still on placing him in his environment.
Wide Shot
WS (Wide Shot)

The subject takes up the full frame, or at least as much as comfortably possible.
AKA: long shot, full shot.
Mid Shot
MS (Mid Shot)

Shows some part of the subject in more detail while still giving an impression of the whole subject.
Medium Close Up
MCU (Medium Close Up)

Half way between a MS and a CU.
Close Up
CU (Close Up)

A certain feature or part of the subject takes up the whole frame.
Extreme Close Up
ECU (Extreme Close Up)

The ECU gets right in and shows extreme detail.
Variation: Choker
cut-in
Cut-In

Shows some (other) part of the subject in detail.
Cutaway
CA (Cutaway)

A shot of something other than the subject.
two-shot
Two-Shot

A shot of two people, framed similarly to a mid shot.
over-the-shoulder shot
(OSS) Over-the-Shoulder Shot

Looking from behind a person at the subject.
noddy
Noddy Shot

Usually refers to a shot of the interviewer listening and reacting to the subject.
point of view (POV)
Point-of-View Shot (POV)

Shows a view from the subject's perspective.
weather shot
Weather Shot

The subject is the weather. Can be used for other purposes, e.g. background for graphics.

Waandishi wakubali kubadilika, wajifunze Kiswahili wasirudie makosa


 


Waandishi wakubali kubadilika, wajifunze Kiswahili wasirudie makosa
 

 

 
 
Na Cosmas Pahalah

KATIKA makala yafuatayo nimetoa maelezo ambayo yana lengo la kusisitiza baadhi ya mambo yaliyoelezwa hapo awali.

 Lengo ni kuimarisha uelewa wa misingi ya lugha sanifu ya Kiswahili. Kwa mfano:
 
“ Misitu ya Kazimzimbwi na Pugu iko katika hatari ya kuvamiwa na wananchi kwa ajili ya kuvuna miti ya kuchomea mkaa.”

Katika sentensi hii msomaji ataelewa kuwa iko miti ya kuchomea mkaa kwa maana ya kuwa miti ni kichocheo cha kuchoma mkaa. Ukweli ni kuwa miti inachomwa na matokeo yake ni upatikanaji wa mkaa. Kwa hiyo, sahihi ni kuandika, “…kwa ajili ya kuvuna miti ya kuchoma mkaa.”

“Kwa bahati nzuri, nilipata fursa ya kuhudhuria mikutano ya kampeni na moja ya mikutano niliyohudhuria ndiyo msingi wa makala hii.”

Ni kawaida kwa maneno yanayoanza na ‘ma’ kama vile mahitaji, madhumuni, maradhi na kadhalika, neno linalofuata kama ni kutoa maelezo ni ‘haya’ kwa mfano, maelezo haya, mahitaji haya, madhumuni haya, maradhi haya n.k. Vivyo hivyo, tunavyoeleza juu ya makala.

Tunasema makala haya na wala siyo makala hii.

Nafahamu kuwa watu wengi wamezoea kuandika makala hii, lakini mazoea yasiwe kisingizio cha kuendeleza makosa.

Ni vigumu kubadilika baada ya kuzoea aina fulani ya mazoea, hivyo hatuna budi kubadilika.

“ Lugha zilizokuwa zikitumiwa na  baadhi yao zilikuwa za kejeli dhidi ya viongozi wa juu wa Chadema.”

Wakati mwandishi alipoandika taarifa hii alisema kuwa wazungumzaji walitumia lugha za kejeli. Ukweli ni kuwa lugha iliyotumika ni ya Kiswahili na wala siyo zaidi. Katika lugha hii, wazungumzaji walitumia maneno ya matamshi ya kejeli na matusi ambayo yalikuwa ni ya udhalilishaji.

Hivyo, ingekuwa bora kama angeandika kuwa wazungumzaji walitumia maneno au matamshi ya kashfa na wala siyo  lugha za kashfa.

“ Kitu kilichomfanya awe na wakati mgumu ni kwa  mpira ilikuwa wa kasi na wenye rafu nyingi.”

Hapa siyo kitu kimoja kichomfanya awe na wakati mgumu bali ni mambo mengi yakiwamo kasi ya mpira na pia rafu nyingi.

Liko neno lililotumika la ‘ilikuwa’ lililotumika kimakosa. Ilitakiwa liwe ‘kuwa’. Kwa hiyo, angeandika,

“Kitu kilichomfanya awe na wakati ngumu ni kwa mpira kuwa wa kasi na wenye rafu.”

“ Hoteli ya Gate Way jana ilinusurika kuvamiwa na  vijana wa Chadema  kufuatia madai kuwa na masanduku ya kura yaliingia katika ngome ya CCM.”

Kwa bahati mbaya mwandishi ana taaluma ndogo ya sarufi kwani ameshindwa kutambua matumizi sahihi ya ‘o’ rejeshi.

Badala ya kuandika ‘masanduku ya kura yaliingia katika ngome ya CCM’ alitakiwa kuandika masanduku ya kura yaliyoingia katika ngome ya CCM.

“Kwa mfano, ukichukua takwimu za wanafunzi kutoka wilayani ukilinganisha na zilizoko mikoani utakuta zinakataana.”

Neno linaloleta mushkeli hapa ni ‘kukataana’. Maana ya kukataa ni kusema au kuonyesha kwa vitendo kutokubali jambo fulani , kusema hapana, kuzuia au kunyima.

Sasa tunaposema kuwa takwimu zimekataana tuna maana ya kunyima, kuzuia au kusema hapana. Maneno yote hayo hayaelekei kukaribia maana iliyokusudiwa.

Neno ambalo lingefaa hapa ni kutofautiana. Kwa maana hiyo, takwimu zilitofautiana kati ya zile za wilayani na zile za mikoani.

Upo mtindo wa waandishi wa magazeti kuendelea kutumia neno maamuzi badala ya uamuzi.

Angalia sentensi zifuatazo ambazo zimetokana na waandishi wawili tofauti na katika nyakati tofauti:
“Haya ndiyo maamuzi magumu ya Pep Guardiala.”

“Hakika hakuna njia nyingine iwapo Jaji huyo, alitoa siri iliyoko kwenye maamuzi kwa mtu mwingine wa pili”.

Kwa kuzingatia uandishi bora, maneno kama maamuzi hayafai kuandikwa kwani yanakiharibu Kiswahili badala ya kukijenga. Tuwe macho kutumia kamusi za Kiswahili ili kuwa na uhakika na kile tunachoandika.

“Askofu Telesphory Mkude alisema hakuna budi kwa Watanzania kuishi katika maisha ya upendo na amani kama ambavyo Mungu alikuwa anawafanyia watu wake.”

Matumizi ya ‘budi’ yanawakanganya watu wengi. Yafaa ieleweke kuwa tunapotumia neno budi tuna maana ya hiyari lakini tunapolitumia hatuna budi, hapana budi, sina budi, hawana budi tuna maana ya kusema ni lazima.

Kwa hiyo, ni muhimu kufahamu kuwa ukisema ni budi niende maana yake una hiyari ya kwenda. Kama ukisema sina budi niende maana yake ni lazima niende.

“Mungu amekuwa akimsamehe kila mtu dhambi zake hususani wale wanaotambua na kumrejea kumwomba awasamehe.”

Kwa kawaida, maneno ya Kiswahili na hata yale yanayotoholewa, yanafuata msingi wa lugha ya Kiswahili usemao kuwa ni lazima kuishia na irabu (a, e, i, o, u).

Hata hivyo, tunayo maneno machache ambayo hayafuati kanuni hii.  Maneno haya ni kama takriban, mathalan, hususan, marmar (marumaru). Orodha ya maneno haya ni fupi lakini ni muhimu kuyajua na kuyatumia ipasavyo.

“Kamati yake inasisitiza kuwa halmashauri zote za Mkoa wa Lindi kutunga sheria ndogo mpya kwa kutambua dhumuni la sheria hizo.”

Katika kipindi kilichopita niwahi kueleza kuwa yako maneno ambayo hayana wingi bali yana umoja tu ijapokuwa neno lenyewe limeanza na kiambishi ma-. Kwa mfano yako maneno kama maji, maradhi, maumivu, madhumuni, maoni na kadhalika ambayo  tunayatumia katika umoja na wingi.

Katika Kiswahili hatuna maneno  kama radhi (maradhi), umivu (maumivu), dhumuni (madhumuni) au oni (maoni). Kama ukiyatumia watakushangaa wajuzi wa lugha ya Kiswahili kwani umeipotosha lugha.

Kwa upande mwingine, tunayo maneno kama ushirikiano na wala siyo mashirikiano, uamuzi na wala siyo maamuzi, shule na wala siyo mashule, upungufu na wala siyo mapungufu, hospitail na wala siyo mahospitali, hoteli na wala siyo mahoteli, benki na wala siyo mabenki, kampuni na wala siyo makampuni

 

 

 

 

 

 

 

MAPISHI

‘FISH FINGER’

 

Karibu sana katika safu hii ya mapishi ambapo leo ninakuletea upishi wa chakula kinachoitwa ‘ Fish Finger’. Ungana nami mtayarishaji wako Cosmas Pahala.

1.     Samaki wakubwa kiasi

2.     Nyanya 5

3.     Hoho 1

4.     Karoti 1

5.     Nyanya kopo 1

6.     Chumvi kiasi

7.     Vitinguu maji na saumu

8.     Mafuta ya kupikia

9.     Pilipili 3

10.                        Ndimu

 

Jinsi ya kupika

 

1.     Kausha vipande vitatu vitatu kwa jua, vikisha kauka visage kwa kutumia blenda (kifaa maalum cha kusagia), vikiwa tayari weak kwenye sahani.

2.   Paka samaki wako chumvi, twanga vitunguu saumu uweke samaki, tia ndimu na maji kiasi.kwenye                                                        

3. Bandika jikoni acha yachemke mpaka maji yote yachemke. Toa miiba ya samaki.

4.     Changanya samaki wako mpaka wachanganyike kabisa kasha viringisha vipande vipande kama vidole.

5.     Weka kwenye ule unga wa mkate ulio kwisha usaga, vunja mayai na tumbukiza vipande kwenye mayai.

6.     Weka mafuta jikoni yapate moto tumbukiza ‘fish finger’ zako ambazo ulizipaka unga wa mkate na mayai.

7.     Acha mpaka ziwe na rangi ya kahawia na uzitoe na kuziweka kwenye chombo kisafi, na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.

 

 

 

 

 

 

SHAIRI

MISAADA YA WAGENI

Wazungu wanayo nongwa, Haki wanatudhulumu

Wanaleta ya paukwa, Twabaki mashamusham

Kila tunacholetewa, Mwishowe twajilaumu

Misaada ya wazungu, Ona inavyo tutesa.

 

Serikali kuelewa, Hii inawalazimu

Misaada mnayopewa, Ndani ndani yake kunabomu

Tusipende vya kupewa, Tukumbuke ya mwalimu

Misaada ya wazungu, Ona inavyotutesa.

 

Kanisa tumeambiwa, Hii ni ya kwetu zamu

Mitumba tunaletewa, Na fedha za kujikimu

Majengo tunajengewa, Ila hili tuheshimu

Misaada ya wazungu, Ona inavyo tutesa.

 

Ndoa ya jinsia sawa, Zifungishwe kwa hakimu

Ndoa ya jinsia sawa, Ati yaitwa karamu

Mwanaume sawasawa, Kuolewa si haramu?

Misaada ya wazungu, Ona inavyo tutesa.

 

Mashehe wetu wazawa, Nawachungaji hudumu

Hii ni chemsha kinywa , Sasa ni yakwetuzamu

Wazee kwetu ni dawa, Tunusuruni kaumu

Misaada ya wazungu, Ona inavyo tutesa

 

 

 

 

 

 

 

 

HUYU NDIYE RAIS TUNAYE MUHITAJI DSJ

Usomi wa ngazi mbalimbali si sifa ya mtu kufaa kuwa kiongozi, dunia katika historia yake ina majina lukuki ya baadhi ya viongozi ambao walikuwa wasomi, lakini hatima ya uongozi wao haikutofautiana na wajinga.

Hata hapa nchini kuna baadhi ya viongozi serikalini, kwenye mashirika na hata kwenye sekta binafsi ambao wakikuonesha vyeti vyao vya shule unaweza kuogopa, lakini utendaji wao ni kichefuchefu.


 

Tukiwa tunaelekea katika uchaguzi mkuu wa viongozi wa serikali ya wanafunzi (DASJOSO), wanafunzi wa DSJ wanatakiwa kuangalia kiongozi ambaye ataweza kuisogeza mbali serikali ya wanafunzi (DASJOSO)  na mwenye uono wa mbali kwa maendeleo ya serikali na chuo kwa ujumla.


Kisaikolijia sifa za kiongozi ziko wazi na ni muhimu, mtu kuwa nazo kabla au baada ya kupewa cheo. Leo tunataka kuziangalia kwa undani sifa hizi, ili kama wanafunzi  wenye dhamana ya kuchagua watu wa kuongoza tuwatazame watu kwa sifa zao kabla na baada ya kuwapa nafasi. Sifa za kiongozi ni hizi zifuatazo:

Awaze mafanikio makubwa
Raisi wa Dasjoso lazima awe na maono ya juu ya kuhakikisha kuwa , serikali ya wanafunzi inapata mafanikio makubwa, hii ndiyo itakuwa dira ya kazi yake itakayompa muongozo wa kusimamia  watendaji wote walio chini yake kufikia kiwango cha mafanikio anachokiwaza. Kiongozi asiyekuwa na mawazo ya juu ya kuendelea kutoka mahali alipo hafai kuongoza.

Awe na nia
Haitoshi kwa Rais kuwa na mawazo chanya peke yake bila kuwa na nia ya kuyatimiza. Hivyo, Rais atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo tu atakuwa na uwezo wa kuratibu vema na kutekeleza alichowaza. Ajue njia anayopita, awatangulie anaowaongoza kwa vitendo.

Ajitambue mwenyewe
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na upungufu wake na awe tayari kujiongezea maarifa kila siku, ili aweze kukabili changamoto na mabadiliko ya ulimwengu. Asome, afuatilie mambo yanavyokwenda na ajifunze kwa wenzake kuhusu kufanikisha malengo yake.

Asimamie maamuzi
Kuna wakati malengo hukumbana na vikwazo, hivyo ni wajibu wa Rais kusimamia maamuzi sahihi na kuwa mtu wa mwisho. Kiongozi mwenye kubadilika badilika kama kinyonga, hafai kwa vile kukosa msimamo kuna maanisha udhaifu wa mipango na kujiamini.

Adhibiti msongo wa mawazo
Tunamtarajia kiongozi mzuri awe ni mtu mwenye kupunguza msongo wa mawazo, ili kuifanya akili yake ifikie maamuzi sahihi, lakini kama atakuwa mwenye kuwaza mengi, atajikuta anachanganyikiwa na kuwa mtu wa jazba katika maamuzi na hivyo kuipotosha jamii.

Akubali kukosolewa
Viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia ya kuthibitisha msimamo wao na usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa kwa kutazama mwenendo wake na usahihi wake. Asiyekubali kukosolewa hafai kuwa kiongozi.


Awe msikilizaji
Rais mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasilikiza watu walio chini yake, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Lakini pia anatakiwa kuwafahamu kwa undani, ili aweze kuwaongoza vema kufuatana na hali zao. Akiwa na watu walemavu wenye kasoro kadhaa wa kadhaa anatakiwa kuwatambua kabla na baada ya kuwa kiongozi wao. Kuongoza usichokifahamu ni ujinga.


Afuate haki
Kiongozi imara anatakiwa kufuata haki katika kuongoza kwake, asijione mwenye haki zaidi ya wale anaowaongoza katika sheria. Ni muhimu kwake kuwafanya walio chini yake kujiona wako huru katika mawazo na matendo. Kiongozi anayetumia nguvu na ukali kuongoza watu hafai. Hata yule mwenye kujivunia uongozi wake naye hafai.

Awe egemeo la watu
Sifa nyingine ya rais ajaye awe egemeo la watu wake katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza, kufurahi pamoja na watu wa chini yake bila kujitenga nao. Ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali na awe tayari kutumika zaidi kwa maslahi ya wengine.

Atie moyo watu


Raisi wa DASJOSO ajaye anatakiwa kuwa na uwezo wa kuwatia moyo walio chini yake ili waweze kuendeleza vipaji vyao. Haipendezi kwa kiongozi kuwavunja moyo watu kwa kauli za kudharau kazi na jitihada zao walizojaribu kufanya katika kutekeleza majukumu yao kama wafanyakazi au wananchi.

Afurahie mafanikio

Sifa nyingine muhimu ya Rais tunaye mtaka awe tayari kufurahia mafanikio aliyopata pamoja na watu wake. Ni wajibu wa kiongozi kutoa tuzo, kuwashukuru wafanyakazi wake na kuwa tayari kuwapa ofa. Hii itasaidia kuwafanya watu waone hawajapoteza nguvu zao katika utendaji wao na kwamba wanakubalika. Si busara wakati mwingine kuwakosoa watu mbele ya hadhara na kueleza kutofurahishwa na kazi zao.


Aungane na wa chini yake

Mtu kuwa Rais haimaanishi amekuwa wa tofauti na watu wengine kiasi cha kushindwa kuchangamana nao kama wanavyofanya baadhi ya viongozi. Rais mwema ni yule atakayeungana na watu wake katika maisha ya kawaida. Kuwa kiongozi haimaanishi kwamba watu watakufuata wewe kila siku, wakati mwingine wewe unatakiwa kuwafuata wao na kuwa nyuma yao hata mahali walipokosea au wanapokabiliwa na makosa, watetee na uoneshe kuwajali na kuwapigania, makosa utayahesabu baada ya utetezi wako kukamilika.



Akubali lawama
Kama Rais akifanya mambo ambayo jamii haikupendezwa nayo anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Ikiwa anaongoza kitego cha umeme kwa mfano na watu hawakupata nishati hiyo kwa wakati hatakiwi kukwepa lawama, vivyo hivyo kwenye wizara na idara au nchi kwa ujumla.

Afahamu kutatua matatizo
Raisi tunaye mwitaji ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo mzuri katika eneo hili umesimama katika mawasiliano na watu wa chini, mawasiliano haya ndiyo yatakayomuwezesha kiongozi kujua matatizo waliyonayo wafanyakazi wake au hata jamii anayoiongoza na hivyo kumfanya apate wasaa wa kuyashughulikia mapema.

Ajifunze kwa makosa
Wakati mwingine mawazo na mipango inaweza ikaenda kombo, hivyo ni wajibu wa Rais atatakiwa kujifunza kutokana na makosa yake au ya wale anaowaongoza, ili kuepuka kurudia makosa yale yale na kumfanya apoteze sifa za kuwa kiongozi mzuri.
Mwanafalsafa Winston Churchill aliwahi kusema "The price of greatness is responsibility." Thamani ya ukuu ni uwajibikaji.



Awe mwaminifu
Miongoni mwa maeneo magumu kabisa yaliyowashinda na yanayoendelea kuwashinda viongozi wengi ni uaminifu. Rais wa DASJOSO anatakiwa awe tayari kusimamia muongozo wa katiba ya nchi au marufuku alizowekewa katika madaraka yake. Hii inakwenda sambamba na kutowaonea, kuwanyanyasa wa nchini yake kwa kutumia cheo chake.

Awe mkweli
Viongozi wengi hasa wa kisiasa siku hizi ni waongo hakuna mfano, wamejaa ahadi zisizotekelezeka na hata wanapogundua kuwa hawana uwezo au wamekwama kuzitimiza, hawaoni haja ya kutubu mbele ya wanaowaongoza. Kiongozi makini ni yule atayekuwa tayari kuonesha ubora wa matendo na kauli zake.

Asiwe mwenye majungu
Kuna baadhi ya viongozi kwenye maofisi wanaendekeza sana majungu na pengine kuyapa umuhimu wa hali ya juu. Hii ni sifa mbaya kwa kiongozi yo yote, hivyo anayetumikia ‘umbea’ katika ofisi aliyokabidhiwa kama mkuu anapaswa kuondolewa. Kiongozi makini atatumia uwezo wake kuzuia watu wasimsengenye/wasisengenyane kwa kuwa muwazi na mwenye kufungua milango ya watu kumuona na kumlaumu na kueleza hisia zao.

Awe bora
Kwa kila analofanya kama rais lazima alifanye kwa ubora, asiwe mtu mwenye kulipua kazi na kufanya chini ya kiwango cha uwezo wake. Kila siku katika kazi, maamuzi, usimamizi, utekelezaji lazima atumike zaidi ya uwezo wake.


Nguzo imara ya mwanafunzi yeyote anayetaka kufanikiwa katika masomo yake ni kuwa mfuasi wa UTII na UAMINIFU mahali popote na kwa mtu yeyote. Nakumbuka wakati nikiwa shule ya sekondari nilikiuka sana mambo haya muhimu, nilikuwa mtu wa vurugu na mwanzilishi wa migomo.

 

 

 

DALILI KUMI NA TATU ZA MIMBA



Na Cosmas Pahalah
MWANAMKE anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida. Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.
“Homoni zinazosambaa mwilini mara tu unapopata ujauzito husababisha mabadiliko kadhaa katika mwili wake ambayo yanaweza kugundulika kabla hata ya uchunguzi halisi wa kujua kama mjauzito au la,” anasema Melissa Goist, Profesa na Mtalaama wa Masuala ya Uzazi wa Chuo Kikuu cha Ohio, Marekani.

Maumivu kwenye matiti
Hii ni dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati yai linavyopata “rutuba”, jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.
Maumivu mwilini
Utaanza kusikia maumivu kama vile unataka kuingia katika siku zako. Kwa kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha maumivu hayo.
Kutokwa damu bila kutegemea
"Wanawake wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao. Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25 ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai,” anasema Goist. Ambaye anaendelea kusema kwamba iwapo utaona hedhi yako inakuwa fupi au inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, unashauriwa kwenda kufanya kipimo cha ujauzito..
Kuchoka
Unapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati ukiwa kazini, lazima ufahamu kwamba mwili wako unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha mabadiliko.
“Tambua kwamba katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza kutumia sehemu ya nguvu zako na hivyo kukuletea uchovu na usingizi” anasema Goist.

Chuchu kuwa nyeusi
Chuchu huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza kufanya kazi kwa nguvu zaidi. Hata hivyo, Goist anasema: “Wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite.”
Kichefuchefu
Hali hii huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa na ujauzito, ambapo nyakati za asubuhi ndipo hasa hujionyesha.
Mwili kuvimba

Kuna wakati kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kukusababishia kuona tumbo limevimba na nguo zikawa zinakubana kutokana na chakula kujaa katika utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema ukatambua kwamba tayari una ujauzito na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.

Kwenda haja ndogo mara kwa mara
Kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu chako kimeanza kufanya kazi ya ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa ujauzito. Hali hii pia hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.
Tamaa ya vitu mbalimbali

Kutokana na mwili kuwa na “mzigo” wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili wake. Hii ni pamoja na kutaka vyakula fulani au kufanya mambo ambayo hapo nyuma alikuwa hayapendi.

Kuumwa kichwa

Kuongezeka kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususani katika wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.

Kufunga choo

Homoni ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo hali hii inaweza kujitokeza zaidi wakati ujauzito unapoendelea kukua.

Kuwa na hasira
"Kutokana na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia uchovu, na kukufanya kuwa na hasira,” anasema Goist
Kuongezeka kwa joto mwilini
Kipimo cha joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna “mtoto anakuja”.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Monday, September 24, 2012

MAKALA GAZETI LA CHUO (MKUFUNZI)


HUYU NDIYE RAIS TUNAYE MUHITAJI DSJ

Usomi wa ngazi mbalimbali si sifa ya mtu kufaa kuwa kiongozi, dunia katika historia yake ina majina lukuki ya baadhi ya viongozi ambao walikuwa wasomi, lakini hatima ya uongozi wao haikutofautiana na wajinga.

Hata hapa nchini kuna baadhi ya viongozi serikalini, kwenye mashirika na hata kwenye sekta binafsi ambao wakikuonesha vyeti vyao vya shule unaweza kuogopa, lakini utendaji wao ni kichefuchefu.


Kisaikolijia sifa za kiongozi ziko wazi na ni muhimu, mtu kuwa nazo kabla au baada ya kupewa cheo. Leo tunataka kuziangalia kwa undani sifa hizi, ili kama wananchi au viongozi wenye dhamana ya kuchagua watu wa kuongoza tuwatazame watu kwa sifa zao kabla na baada ya kuwapa nafasi. Sifa za kiongozi ni hizi zifuatazo:

Awaze mafanikio makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono ya juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake sekta yake inapata mafanikio makubwa, hii ndiyo itakuwa dira ya kazi yake itakayompa muongozo wa kusimamia wafanyakazi na watendaji wote walio chini yake kufikia kiwango cha mafanikio anachokiwaza. Kiongozi asiyekuwa na mawazo ya juu ya kuendelea kutoka mahali alipo hafai.

Awe na nia
Haitoshi kwa kiongozi kuwa na mawazo chanya peke yake bila kuwa na nia ya kuyatimiza. Hivyo, kiongozi atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo tu atakuwa na uwezo wa kuratibu vema na kutekeleza alichowaza. Ajue njia anayopita, awatangulie anaowaongoza kwa vitendo.

Ajitambue mwenyewe
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na upungufu wake na awe tayari kujiongezea maarifa kila siku, ili aweze kukabili changamoto na mabadiliko ya ulimwengu. Asome, afuatilie mambo yanavyokwenda na ajifunze kwa wenzake kuhusu kufanikisha malengo yake.

Asimamie maamuzi
Kuna wakati malengo hukumbana na vikwazo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kuwa mtu wa mwisho. Kiongozi mwenye kubadilika badilika kama kinyonga, hafai kwa vile kukosa msimamo kuna maanisha udhaifu wa mipango na kujiamini.

Adhibiti msongo wa mawazo
Tunamtarajia kiongozi mzuri awe ni mtu mwenye kupunguza msongo wa mawazo, ili kuifanya akili yake ifikie maamuzi sahihi, lakini kama atakuwa mwenye kuwaza mengi, atajikuta anachanganyikiwa na kuwa mtu wa jazba katika maamuzi na hivyo kuipotosha jamii.

Akubali kukosolewa
Viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia ya kuthibitisha msimamo wao na usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa kwa kutazama mwenendo wake na usahihi wake. Asiyekubali kukosolewa hafai kuwa kiongozi.


Awe msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasilikiza watu walio chini yake, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Lakini pia anatakiwa kuwafahamu kwa undani, ili aweze kuwaongoza vema kufuatana na hali zao. Akiwa na watu walemavu wenye kasoro kadhaa wa kadhaa anatakiwa kuwatambua kabla na baada ya kuwa kiongozi wao. Kuongoza usichokifahamu ni ujinga.


Afuate haki
Kiongozi imara anatakiwa kufuata haki katika kuongoza kwake, asijione mwenye haki zaidi ya wale anaowaongoza katika sheria. Ni muhimu kwake kuwafanya walio chini yake kujiona wako huru katika mawazo na matendo. Kiongozi anayetumia nguvu na ukali kuongoza watu hafai. Hata yule mwenye kujivunia uongozi wake naye hafai.

Awe egemeo la watu
Sifa nyingine ya kiongozi ni kuwa egemeo la watu wake katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza, kufurahi pamoja na watu wa chini yake bila kujitenga nao. Ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali na awe tayari kutumika zaidi kwa maslahi ya wengine.

Atie moyo watu
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuwatia moyo walio chini yake ili waweze kuendeleza vipaji vyao. Haipendezi kwa kiongozi kuwavunja moyo watu kwa kauli za kudharau kazi na jitihada zao walizojaribu kufanya katika kutekeleza majukumu yao kama wafanyakazi au wananchi.

Afurahie mafanikio

Sifa nyingine muhimu ya kiongozi ni kuwa tayari kufurahia mafanikio aliyopata pamoja na watu wake. Ni wajibu wa kiongozi kutoa tuzo, kuwashukuru wafanyakazi wake na kuwa tayari kuwapa ofa. Hii itasaidia kuwafanya watu waone hawajapoteza nguvu zao katika utendaji wao na kwamba wanakubalika. Si busara wakati mwingine kuwakosoa watu mbele ya hadhara na kueleza kutofurahishwa na kazi zao.


Aungane na wa chini yake

Mtu kuwa kiongozi haimaanishi amekuwa wa tofauti na watu wengine kiasi cha kushindwa kuchangamana nao kama wanavyofanya baadhi ya viongozi. Kiongozi mwema ni yule atakayeungana na watu wake katika maisha ya kawaida. Kuwa kiongozi haimaanishi kwamba watu watakufuata wewe kila siku, wakati mwingine wewe unatakiwa kuwafuata wao na kuwa nyuma yao hata mahali walipokosea au wanapokabiliwa na makosa, watetee na uoneshe kuwajali na kuwapigania, makosa utayahesabu baada ya utetezi wako kukamilika.



Akubali lawama
Kama kiongozi amefanya mambo ambayo jamii haikupendezwa nayo anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Ikiwa anaongoza kitego cha umeme kwa mfano na watu hawakupata nishati hiyo kwa wakati hatakiwi kukwepa lawama, vivyo hivyo kwenye wizara na idara au nchi kwa ujumla.

Afahamu kutatua matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo mzuri katika eneo hili umesimama katika mawasiliano na watu wa chini, mawasiliano haya ndiyo yatakayomuwezesha kiongozi kujua matatizo waliyonayo wafanyakazi wake au hata jamii anayoiongoza na hivyo kumfanya apate wasaa wa kuyashughulikia mapema.

Ajifunze kwa makosa
Wakati mwingine mawazo na mipango inaweza ikaenda kombo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kujifunza kutokana na makosa yake au ya wale anaowaongoza, ili kuepuka kurudia makosa yale yale na kumfanya apoteze sifa za kuwa kiongozi mzuri.
Mwanafalsafa Winston Churchill aliwahi kusema "The price of greatness is responsibility." Thamani ya ukuu ni uwajibikaji.



Awe mwaminifu
Miongoni mwa maeneo magumu kabisa yaliyowashinda na yanayoendelea kuwashinda viongozi wengi ni uaminifu. Kiongozi bora ni yule ambaye yuko tayari kusimamia muongozo wa katiba ya nchi au marufuku alizowekewa katika madaraka yake. Hii inakwenda sambamba na kutowaonea, kuwanyanyasa wa nchini yake kwa kutumia cheo chake.

Awe mkweli
Viongozi wengi hasa wa kisiasa siku hizi ni waongo hakuna mfano, wamejaa ahadi zisizotekelezeka na hata wanapogundua kuwa hawana uwezo au wamekwama kuzitimiza, hawaoni haja ya kutubu mbele ya wanaowaongoza. Kiongozi makini ni yule atayekuwa tayari kuonesha ubora wa matendo na kauli zake.

Asiwe mwenye majungu
Kuna baadhi ya viongozi kwenye maofisi wanaendekeza sana majungu na pengine kuyapa umuhimu wa hali ya juu. Hii ni sifa mbaya kwa kiongozi yo yote, hivyo anayetumikia ‘umbea’ katika ofisi aliyokabidhiwa kama mkuu anapaswa kuondolewa. Kiongozi makini atatumia uwezo wake kuzuia watu wasimsengenye/wasisengenyane kwa kuwa muwazi na mwenye kufungua milango ya watu kumuona na kumlaumu na kueleza hisia zao.

Awe bora
Kwa kila analofanya kama kiongozi lazima alifanye kwa ubora, asiwe mtu mwenye kulipua kazi na kufanya chini ya kiwango cha uwezo wake. Kila siku katika kazi, maamuzi, usimamizi, utekelezaji lazima atumike zaidi ya uwezo wake.

























Nguzo imara ya mwanafunzi yeyote anayetaka kufanikiwa katika masomo yake ni kuwa mfuasi wa UTII na UAMINIFU mahali popote na kwa mtu yeyote. Nakumbuka wakati nikiwa shule ya sekondari nilikiuka sana mambo haya muhimu, nilikuwa mtu wa vurugu na mwanzilishi wa migomo.

Wakati huo sikuona kama nilikuwa nafanya makosa, mara zote nilijitazama kama shujaa kwa vile jamii, walimu na wanafunzi wenzangu walikuwa wakiniogopa. Kifupi nilikuwa na akili darasani lakini matokeo ya mwisho yalipotoka yalinishangaza kwani nilifeli.

Kushindwa huko kulinirudisha kwenye mikono ya wazazi ambao tayari nao nilikuwa nimewachosha kwa tabia zangu. Toka hapo hakuna mjomba wala shangazi aliyejitokeza kunisaidia kimasomo kwa kuwa sikuwa mtu wa kuaminiwa. Nilikaa nyumbani kama mtu muhuni kwa miaka mitano hadi nilipokubali kubadili tabia yangu.

Nilifikia uamuzi huo kwa sababu nilinusurika kufungwa jela baada ya kushiriki katika ugomvi ulioleta harufu ya mauaji ya kijana mmoja tuliyekuwa tukigombana naye. Nililazimika kutoroka na kukaa uhamishoni kwa miaka kadhaa. Baadaye nilikutana na maisha magumu ambayo siwezi kuyasahau.

Nakumbuka wakati huo wa dhiki nilijutia utundu nilioufanya shule kwa kuchezea elimu na kujikita katika mambo ya kihuni ambayo hayakunisaidia. Mwezi wa nane mwaka 1998 nilikubali kubadilika na kuanza kujifunza upya maisha ya utii na uaminifu chini ya uongozi wa walimu wa dini yangu ya kikristo.

Mafundisho ya kidini yalinisaidia kuacha ulevi na uvutaji wa sigara. Marekebisho hayo ya tabia yalinijenga zaidi upande wa rafiki zangu niliokuwa nasali nao, lakini ndugu walikuwa bado wananitilia shaka. Rafiki zangu hawakupata shida tena kunituma kusimamia ujenzi wa nyumba zao na miradi yao na mara nyingine niligeuka kuwa ‘benki’ nikawa natunza pesa za watu.

Simulizi ni ndefu lakini mwisho wa yote uaminifu wangu huo ndiyo uliomsukuma mmoja kati ya rafiki zangu kujitolea kunisomesha masomo ya jioni ili nirudie masomo niliyofeli nilipopata nafasi hiyo sikuichezea kwani tayari nilikuwa nimeonja machungu ya ujinga. Nilijituma kusoma kwa malengo na kufanikiwa kusahihisha cheti changu.

Nilipomaliza nilichagua fani ya uandishi wa habari, ambapo alitokea mama mmoja niliyemheshimu na kumtii akanisaidia tena kunisomesha. Kifupi maisha yangu yalikuwa ya kubebwa na watu niliowaonesha uaminifu na utii wangu.

Hawa ni rafiki zangu wa hapa nchini achilia mbali Dr ………………… kutoka chuo cha American Psychology ambaye alijitolea kunifundisha masomo ya Saikolojia elimu ambayo ilinifumbua macho na kuniwezesha kuwa hivi nilivyo sasa.

Huu ni ushuhuda wangu kwa ufupi, ambao nimeutoa kwa lengo la kuwafundisha kwa vitendo nguvu ya uaminifu na utii katika maisha ya kila siku ya mwanadamu na hasa kwa wanafunzi ambao safari ya kupata elimu inahitaji ushirikiano wa watu wanaoishi nao nyumbani na shuleni.

Wanafunzi wengi wameshindwa kufanikiwa kwa sababu ya kutokuwa waaminifu na watii kama nilivyoeleza huko nyuma, jambo ambalo limewafanya watengwe na jamii mithili ya yale yaliyonitokea mimi.

Ifahamike kuwa mwanafunzi hawezi kupata msaada wa kutosha kwa wazazi, walimu na ndugu zake kama atakuwa akipewa ada anaitumia vibaya, akiwa na kashfa za ngono, wizi, uvutaji bangi na utumiaji wa dawa za kulevya na kuonesha ukorofi.

MADA HII INAENDELEA UNAWEZA KUIPATA KWA KIREFU KAMA UTANUNU KITAMBU CHANGU CHA SAIKOLOJIA MBINU 100 ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI. KINAUZWA NA WAUZA MAGEZETI NCHI NZIMA



















DALILI KUMI NA TATU  ZA MIMBA



MWANAMKE anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida. Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.
“Homoni zinazosambaa mwilini mara tu unapopata ujauzito husababisha mabadiliko kadhaa katika mwili wake ambayo yanaweza kugundulika kabla hata ya uchunguzi halisi wa kujua kama mjauzito au la,” anasema Melissa Goist, Profesa na Mtalaama wa Masuala ya Uzazi wa Chuo Kikuu cha Ohio, Marekani.

Maumivu kwenye matiti
Hii ni dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati yai linavyopata “rutuba”, jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.
Maumivu mwilini
Utaanza kusikia maumivu kama vile unataka kuingia katika siku zako. Kwa kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha maumivu hayo.
Kutokwa damu bila kutegemea
"Wanawake wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao. Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25 ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai,” anasema Goist. Ambaye anaendelea kusema kwamba iwapo utaona hedhi yako inakuwa fupi au inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, unashauriwa kwenda kufanya kipimo cha ujauzito..
Kuchoka
Unapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati ukiwa kazini, lazima ufahamu kwamba mwili wako unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha mabadiliko.
“Tambua kwamba katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza kutumia sehemu ya nguvu zako na hivyo kukuletea uchovu na usingizi” anasema Goist.

Chuchu kuwa nyeusi
Chuchu huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza kufanya kazi kwa nguvu zaidi. Hata hivyo, Goist anasema: “Wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite.”
Kichefuchefu
Hali hii huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa na ujauzito, ambapo nyakati za asubuhi ndipo hasa hujionyesha.
Mwili kuvimba

Kuna wakati kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kukusababishia kuona tumbo limevimba na nguo zikawa zinakubana kutokana na chakula kujaa katika utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema ukatambua kwamba tayari una ujauzito na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.

Kwenda haja ndogo mara kwa mara
Kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu chako kimeanza kufanya kazi ya ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa ujauzito. Hali hii pia hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.
Tamaa ya vitu mbalimbali

Kutokana na mwili kuwa na “mzigo” wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili wake. Hii ni pamoja na kutaka vyakula fulani au kufanya mambo ambayo hapo nyuma alikuwa hayapendi.

Kuumwa kichwa

Kuongezeka kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususani katika wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.

Kufunga choo

Homoni ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo hali hii inaweza kujitokeza zaidi wakati ujauzito unapoendelea kukua.

Kuwa na hasira
"Kutokana na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia uchovu, na kukufanya kuwa na hasira,” anasema Goist
Kuongezeka kwa joto mwilini
Kipimo cha joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna “mtoto anakuja”.