Tuesday, June 12, 2012

IDARA YA HABARI NA WASEMAJI WA WIZARA, TAASISI NA HALMASHAURI ZA WILAYA NA MIKOA WATAKIWA KUJIPANGA KATIKA KUISEMEA SERIKALI


  IDARA ya Habari ( MAELEZO) imetakiwa kujipanga  vizuri ili kuweza kutekeleza majukumu yake ya kuwa Msemaji wa    Serikali ipasavyo; hatua hiyo itasaidia kuepusha malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusiana na utendaji wa Serikali.
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara wakati akifungua kikao kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali katika ukumbi wa Victoria Palace Jijini Mwanza.
Aidha, Dkt. Mukangara alisema, Idara ya Habari ( MAELEZO) ina jukumu zito la kuwa Msemaji  Mkuu wa Serikali . Hii ni kwa mujibu wa agizo la Serikali Na. C 16 la mwaka  1977.
" Serikali inafanya mambo mengi  mazuri kwa wananchi lakini hayasemwi. Matokeo yake Serikali inaishia kulaumiwa na wananchi bila sababu.
"Ndugu zangu hali hii haikubaliki. Lazima tubadilike na lazima tuseme . Hatuwezi kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali asiyesema." Alisema Dkt. Mukangara.
Dkt. Mukangara aliongeza kuwa Idara ya habari itekeleze jukumu hilo kwa kushirikiana na Wasemaji wa Wizara na Taasisi mbalimbali  za Serikali na Wasemaji hao watambue kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ni Idara ya Habari.
Akizungumzia  kuhusu uhuru wa vyombo vya habari alisema,tunalo tatizo la baadhi ya vyombo vya habari  nchini kudhani kwamba uhuru wa vyombo vya habari hauna mipaka. Hivyo alivitaka vyombo vya  habari vitambue kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo utendaji wa vyombo vyake vya habri haubna mipaka.
" Wakati wote uhuru wa vyombo vya habari  popote pale huendana na wajibu hata ktika mataifa yaliyoendelea"Alisema Dkt. Mukangara.
Aidha, alivitaka vyombo vya habari kuwa makini katika kutangaza habari zinazohusu mchakato wa mabadiliko ya katiba huku akisissitiza kuonyesha uzalendo wa hali ya juu katika kuwahabarisha wananchi na kutoa elimu.

 
Dkt. Mukangara pia aliwataka Maafisa  hao kuhakikisha kwamba wanaelimisha wananchi  juu ya umuhimu wa zoezi la Sensa ya watu na Makazi.
Baadhi ya mada zitakazojadiliwa katika kikao hicho cha siku tano chini ya Uenyekiti wa  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Sethi Kamuhanda, ni pamoja na Changamoto za utaratibu wa usajili wa magazet; Changamoto zinazoikabili Tanzania katika kuhama  kutoka Analojia kwenda Digitali kufikia mwaka 2012; Wajibu wa Maafisa Mawasiliano na mfumo wa mawasiliano Serikalini; na  Kazi za Serikali Mtandao na Tovuti kuu.
Kwa upande wake Afisa Habari  wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Bi Monica Mutoni  alisema kikao kazi hiki ni fursa kwa Maafisa Habari kuboresha kazi zao  na kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuwahabarisha wananchi majukumu ya Serikali.
Naye Afisa Habari wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Bw. Leonidas Tibanga alisema kuwa baada ya kikao kazi hicho,  Maafisa Habari wataweza kupata ujuzi mpya kutokana na mada zitakazotolewa, na kubadilishana uzoefu ikiwa ni pamoja na kuongeza wigo wa mawasiliano miongoni mwao.
Vikao kazi vya Maafisa Habari vimekuwa vikifanyika kila mwaka  chini ya uratibu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamduni na Michezo ili kujadili namna bora ya utoaji habari za Serikali na uimarishaji wa mawasiliano kwa umma

day, June 12, 2012

BASATA: WASANII JIPANGENI KUHIMILI USHINDANI WA KIMATAIFA

 
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka wasanii kujipanga kwa ajili ya kuhimili ushindani wa kimataifa kutokana na ujio wa mfumo wa digitali ambao utazifanya kazi zao kuonekana kimataifa.

Wito huo umetolewa wiki hii kwenye ukumbi wa BASATA na Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Ghonche Materego wakati akihitimisha mjadala kwenye Jukwaa la Sanaa uliohusu Teknolojia ya Digital na Faida Zake Katika Sekta ya Sanaa uliochokozwa na Mhandisi Joel Chacha kutoka mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (Tcra).

Alisema kuwa, mfumo wa digitali utaruhusu uwepo wa vituo vingi vya redio na runinga ambavyo vitakuwa na masafa ya kimataifa hivyo ni wazi wasanii wanatakiwa kujipanga katika kuandaa maudhui bora, ya kutosha na yenye mvuto kwa ajili ya kukidhi ongezeko hilo na zaidi ushindani wa kimataifa.

“Wasanii tujipange, fursa zinazokuja ni nyingi mno, zinahitaji maudhui ya kutosha, yenye ubora na yatakayoweza kuvifanya vyombo vya habari viweze kuhimili ushindani pia” alisisitiza Materego.
Aliongeza kuwa, moja ya eneo ambalo limekuwa likilalamikiwa na wamiliki wa vyombo vya habari ni uhafifu wa maudhui ya kazi za Sanaa hivyo, wasanii hawana budi kuacha kulalamika na kujipanga kukabili changamoto hiyo.
Awali akiwasilisha mada hiyo,Mhandisi Chacha alisema kuwa, mfumo wa digitali utazalisha fursa nyingi katika sekta ya Sanaa lakini akasisitiza kuwa, uchangamfu wa Wasanii wetu ndiyo utawafanya wafaidi.
Alizitaja baadhi ya fursa hizo kuwa ni pamoja na; ongezeko la ajira kwa Wasanii, ongezeko la vipindi, kukua kwa ushindani katika ubunifu na utengenezaji maudhui yenye ubora, Sanaa za Tanzania kutangazika kimataifa na kuongezeka kwa makampuni yatakayojihusisha na sekta ya Sanaa
“Mfumo wa digitali una mazuri mengi lakini kubwa ni kuongezeka ushindani na ubora katika kutengeneza maudhui yenye ubora na pia ongezeko la masafa katika televisheni ambayo yatahitaji maudhui (vipindi) ya kutosha” Aliongeza Chacha.

Hata hivyo, aliitaja changamoto ya uharamia kwenye sekta ya Sanaa ambapo aliwashaiuri wasanii kuamka na kujiunga na Chama cha hakimiliki (Cosota) ili kuhakikisha kazi zao zinalindwa kisheria.

Wadau wengi waliochangia mjadala huo walionekana kuwa na wasiwasi na mfumo wa digitali lakini wakaomba elimu ya kutosha itolewe ili wananchi wengi zaidi waelewe nini maana ya kutoka mfumo wa analogia kwenga ule wa digitali.

EURO 2012 NEWS: UKRAINE YAIKUNG'UTA SWEDEN 2-1

EURO 2012 NEWS: UKRAINE YAIKUNG'UTA SWEDEN 2-1

SWEDEN 
 ZLATAN IBRAHIMOVIC AKISHANGILIA

UKRAINE

MATCH FACTS:

Ukraine: Pyatov, Gusev, Mykhalyk, Khacheridi, Selin, Yarmolenko, Tymoschuk, Konoplianka (Devic 90), Nazarenko, Voronin (Rotan 84), Shevchenko (Milevskiy 81).
Subs Not Used: Koval, Kucher, Garmash, Aliev, Shevchuk, Seleznyov, Rakitskiy, Butko, Goryainov.
Goals: Shevchenko 55, 62.
Sweden: Isaksson, Lustig, Mellberg, Granqvist, Martin Olsson, Elm, Kallstrom, Larsson (Wilhelmsson 69), Ibrahimovic, Toivonen (Svensson 63), Rosenberg (Elmander 71).
Subs Not Used: Wiland, Jonas Olsson, Hysen, Antonsson, Wernbloom, Safari, Holmen, Bajrami, Hansson.
Booked: Kallstrom, Elm.
Goal: Ibrahimovic 52.
Attendance: 68,000
Referee: Cuneyt Cakir (Turkey)

WAMWAGA BOB MAKANI

WAMWAGA BOB MAKANI


R
AIS Jakaya Kikwete ameongoza mamia ya waombolezaji kutoa heshima za mwisho kwa mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Bob Makani (76), aliyefariki dunia Jumamosi iliyopita.

Akizungumza katika shughuli hiyo, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam, Rais Kikwete amesema mchango wa hayati Makani hasa katika nyanja za kisiasa na kiuchumi utakumbukwa daima na Watanzania.


Katika hotuba yake fupi, Rais ameeleza jinsi alivyozipata taarifa za msiba huo mkubwa na jinsi alivyoguswa kwa kumpoteza mwanasiasa mkongwe....

Akimzungumzia hayati Makani, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema alikuwa ni mwanasiasa mahiri na mkweli, lakini mfumo wa kisiasa Tanzania haukumpa fursa ya kupata nafasi ya uongozi kitaifa.

Amesema, Makani aligombea ubunge zaidi ya mara mbili lakini hakuwahi kushinda kwa kile ambacho Mbowe alidai kuwa ni tatizo la mfumo.

Katika hotuba yake, Mbowe alimkumbuka nyakati muhimu za marehemu Makani alizowahi kuzishuhudia ikiwemo kutoa hotuba fupi kuliko zote katika moja ya kampeni zake za kugombea ubunge huko Shinyanga.

Kwa upande wake Mwasisi wa Chadema, Edwin Mtei aliyeanzisha chama hicho pamoja na Makani amesema taifa limepoteza nguzo imara wakati huu likiwa katika mchakato wa mabadiliko muhimu ya nchi.

Hotuba hiyo ya Mtei iliyosomwa kwa niaba yake na Mzee wa Chadema, Victor Kimesera ilieleza historia ya wawili hao wakiwa wanafunzi katika Shule ya Sekondari Tabora na baadaye wafanyakazi wa BoT.

Naye Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaja marehemu Makani kuwa mtu jasiri ambaye alianzisha chama cha upinzani hasa enzi zile ambazo upinzani ulionekana kama uhaini... “Alikuwa ni mtu ambaye haogopi, alisema hadharani kile alichokiona kinafaa.”

Dk Slaa amesema japokuwa Makani alikuwa mgonjwa na umri wake kuwa mkubwa, lakini bado aliendelea kufanya kazi za chama bila makosa

HISTORIA YA FREEMASONS



HISTORIA YA KALE HADI FREEMASONS
Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza ni kwanini majina ya miungu wa kigiriki na wale wa Kirumi, ambao ustaarabu wao pia umechanulia mashariki ya kati ilikuwa ikiyatumia majina ya sayari kama majina ya miungu yao?
Walizijua vipi sayari hizo na majina yake enzi hizo za maelfu ya miaka kabla ya Masihi?. Nia yangu si kupatiwa majibu lakini kilicho kikubwa ni kwamba millennia nyingi wakati wa mpango  mkubwa wa kuichukua dunia ili iwe ya kabila fulani moja tu; 
Taarifa nyingi kuhusu historia ya kweli ya dunia zimekuwa zikifichwa na kupewa watu maalum kama ambavyo tutakavyoona huko mbele.
Kutufundisha kwamba binadamu wa kwanza alikuwa NYANI aliyeishi mamilioni ya miaka mingi huko nyuma na kwamba nyani huyo alianza kubadilika taratibu hadi akapatikana tunayemwita BINADAMU leo; hiyo yote ni sehemu ya kututupilia mbali na ukweli wa mambo.
Kwa maelfu ya miaka dunia imekuwa ikipitia mabadiliko na misukosuko kadhaa lakini hakuna hata moja lililopata kuelezewa na wale wanaoitwa WANAHISTORIA kwasababu si kazi yao.
Kazi yao ni kufundisha kile tu walichoambiwa na kuelekezwa wakifundishe. Masalio mengi ya kihistoria, yaliyopatikana miaka ya hivi karibuni ngesaidia kuibadili historia inayotumika hivi sasa. Kinachoshangaza yamewekwa kama mapambo kwenye majumba ya makumbusho.
Mfumo mzima wa elimu umeshikiliwa na KABILA HILO LA WAVAMIZI wanafahamu kipi kifundishwe kwenye Kemia , Baiolojia, Fizikia, Hisabati, Historia na fani nyingine mbalimbali.
Kwa miaka mingi sasa mfumo wa elimu umekuwa wa kukitukuza kile kilochofanywa na wasomi waliotangulia, wala hautoi nfasi kwa wasomi wa sasa nao kuwa wabunifu na hivyo kuleta maarifa mapya.
KWANINI?
Mtu kunakili kilichoandikwa kitabuni anaonekana kuwa na akili sana na mtu anayeelewa vyema somo.; Yule nayejaribu kuelezea kwa maneno yake ili kuonyesha ubunifu wake wa namna alivyolielewa somo husika nje ya mstari na nukta za vitabuni anaonekana hajui kitu kwa hiyo amekosea.
Huo ndio mfumo uliotengeneza tangu enzi na enzi ili kufanya binadamu awe mjinga maisha yake yote ili hali mkononi anacho cheti kinachomtambulisha kuwa ana shahada moja, mbili, tatu hata nne. Lakini kichwani mwake ni kama maktaba iliyojaa vitabu vilivyoandikwa na wengine.
Vitabu vyenye maneno na mawazo ya watu ambayo kwa miaka yote waliyokuwa shuleni walilazimishwa kuvikariri kama vilivyo na hakuna jipya waliloondoka nalao kwa kifupi hakuna lake hata moja! Je huyu kweli ni msomi au kabati la vitabu?.
MBINU kubwa waliyoitumia ana ambayo bado inatiliwa msisitizo kwa njia mbalimbali ni kuwafanya watu wa makabila mengine waendelee kuwa WAJINGA na WAPUMBAVU wa mwisho kabisa. Elimu na yale maarifa ya ukweli, wakayachukua wao.
KWA LEO NIISHIE HAPA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Wednesday, June 6, 2012

FREEMASONS AND TANZANIA GOVERNMENT

001~7.jpg 10 views
015~2.jpg 21 viewsGrant of the Dignity of an Honorary Knight Commander of the Civil Division of the Order of the British Empire signed by Queen Elizabeth II and Prince Philip, the Duke of Edinburgh – 2003.
004~8.jpg 17 viewsAndy with Presidents Nyerere and Mkapa at the reopening of Manyoni / Singida railway line 1997.
003~13.jpg 340 viewsAndy at a reception hosted by Provincial Grand Master of Nigeria, Irish Constitution, Lagos 1990.
019~0.JPG 37 viewsAndy Chande with President Julius Nyerere on his visit to Chande Industries Ltd, 1965.
021~1.jpg 49 viewsAndy with Tanzania’s Minister for Foreign Affairs Benjamin William Mkapa (Later the Republic's President) -1969.
042.JPG 46 viewsAndy Chande with Minister for Health, Republic of Seychelles, 2002.
054.jpg 50 viewsAndy Chande with President Amani Abeid Karume of Zanzibar. 2007.

Last additions
045_211x300.jpg 38 viewsGG2 AwardsJul 17, 2011
040_207x451.jpg 32 viewsNRI Dinner December 2008.Jul 17, 2011
039_192x300.jpg 40 viewsLifetime Achievement Award presented by Sarah Brown Wife of U.K. Prime Minister September 2008, London.Jul 17, 2011
051.jpg 86 viewsAndy Chande with The Hon. Frederick Sumaye Prime Minister of Tanzania 2005.May 28, 2011
049.jpg 70 viewsAndy Chande with Daniel Hays Speaker of Senate of Canada – 2005.May 28, 2011
045.jpg 80 viewsAndy and Jayli Chande with Minister for Natural Resources and Tourism Mr Tungaraza – 2003.May 28, 2011
044.jpg 69 viewsAndy Chande President Ali Hassan Mwinyi and British High Commissioner Richard Clarke 2003.May 28, 2011
035.jpg 82 viewsAndy Chande with second President of Tanzania Ali Hassan Mwinyi 1998.May 28, 2011

010~2.jpg 21 viewsThe Guardian: 10th March 2010 - Nigeria's High Commissioner to Tanzania, Ishaya Samaila Majanbu, reads Queen Elizabeth 11's 61st Commonwealth Day anniversary message at a function in Dar es Salaam on Monday night. Others are Royal Commonwealth Society Honorary representative Andy Chande (L) and Mwalimu Nyerere Foundation Chairman Salim Ahmed Salim ( Photo: Selemani Mpochi).
003~4.jpg 31 viewsBangalore Kidney Foundation, Chande Kidney Centre at Padmanabhanagar, Bangalore, India.1990.
007~4.jpg 44 viewsPresident J M Kikwete presenting IMTU charter and certificate, to the Chancellor of IMTU, Sir Andy Chande,KBE, to the right of the President is the then Minister for Education and Vocational Training Professor Jumanne Maghembe – 2010.
008_225x300.jpg 12 viewsABI USA - World Lifetime Achievement – 1999.
018.jpg 18 viewsAndy making Presentation to the Amir of Kano accompanied by District Governor Abdulrahman O Funsho 1996.
005~7.jpg 9 views Andy and Jayli Chande with National President of Round Table Finland and his wife Helsinki 1969.
001~13.jpg 12 viewsAndy, Chairman Tanzania Railways Corporation with his colleagues joining Tourists at the First trip by a 1953 British built Steam Locomotive named Suk ( after a tribe in Kenya). The Excursion Train Service began in 1996 took tourists on seven hours round trip for Dar es Salaam-Soga-Dar es Salaam.
014~4.jpg 41 viewsAndy Chande with President Nyerere at a Chambers of Commerce dinner. Andy’s college Alan Nihill and James Ritchie are on his left, 1964.


045_211x300.jpg 38 viewsGG2 AwardsJul 17, 2011
040_207x451.jpg 32 viewsNRI Dinner December 2008.Jul 17, 2011
039_192x300.jpg 40 viewsLifetime Achievement Award presented by Sarah Brown Wife of U.K. Prime Minister September 2008, London.Jul 17, 2011
051.jpg 86 viewsAndy Chande with The Hon. Frederick Sumaye Prime Minister of Tanzania 2005.May 28, 2011
049.jpg 70 viewsAndy Chande with Daniel Hays Speaker of Senate of Canada – 2005.May 28, 2011
045.jpg 80 viewsAndy and Jayli Chande with Minister for Natural Resources and Tourism Mr Tungaraza – 2003.May 28, 2011
044.jpg 69 viewsAndy Chande President Ali Hassan Mwinyi and British High Commissioner Richard Clarke 2003.May 28, 2011
035.jpg 82 viewsAndy Chande with second President of Tanzania Ali Hassan Mwinyi 1998.May 28, 2011