Saturday, May 26, 2012

Wataalamu wa afya ni nyenzo muhimu katika maisha yetu


Na Cosmas J. Pahalah

Wataalamu wa afya ni nyenzo muhimu katika maisha yetu ya kila siku kutokana na mchango wao kutibu magonjwa mbalimbali kwenye miili yetu

Ili tuweze kutimiza hadhima yao wadau,Serikali na taasisi mbalimbali Nchini zinatakiwa ziwaunge mkono kwakutambua umuhimu wa kazi zao ili waweze kusogeza huduma hizo kwa Wananchi.

Dkt Kefa Omary kutoka kituo cha Medical Missionaries Lifestyle centre ni mmoja katia ya wataalamu wanaotibu  magonjwa zaidi ya kumi kwa kuwaelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kula matunda,juisi pamoja na chakula bora ili waepukane na magonjwa nyemelezi kwenye miili yetu.

Anasema kuwa huduma hiyo yakuwaelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kula vyakula bora wanaitoa bure kwa Wananchi ikiwa ni moja kati ya mipango mikakati ya kituo hicho.

Hata hivyo anasema kuwa magonjwa anayotibu na kwakuwaelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kula vyakula bora,pamoja nakufuata sheria nane za Afya(NEWSTART). Baadhi ya magonjwa anayo yatibu  ni vidonda vya tumbo,kisukari,saratani,presha yakupanda na kushuka,pamoja na matatizo ya uzazi,kiarusi,figo,prostrate,macho, kifafa, fungus, ini ,chango, pumu na kupunguza unene.

Anasema kuwa Kituo hicho kinatoa elimu kupitia makanisa,shule,vyuo ili kuleta hamasa kwa Wananchi kujua umuhimu wa kula vyakula,juisi pamoja na matunda ili waepukane na magonjwa ya mlipuko.

Pia hutoa elimu  kupitia  makongamano na maonesho mbalimbali ndani na nje ya nchi, kama vile maonesho ya sabasaba, na kongamano la vijana katika chuo kikuu cha Sokoine nakatika chuo kikuu cha Rwanda, BARATON kilichopo nchini Kenya.

Hata hivyo anasema kuwa katika kuhakikisha huduma hiyo inawafikia Wananchi kituo kinategeme Chuo kitakachojulikana kwa jina la Medical Missinaries Life Style Centre kutoa elimu kwa wananchi

“Taasisi yetu ipo chini ya chuo cha Lomalinda kilichopo nchini Marekani; pia kuna matawi mengine ambayo ni chuo cha Kibidura kilichipo  Iringa pamoja na River side kilichopo Zambia, ikiwa ni moja ya harakati zetu katika kuhakikisha elimu hii ya kula vyakula bora pamoja na juisi inawafikia Wananchi”.

Anasema kuwa licha ya kituo hicho kutoa elimu juu ya umuhimu wa kula vyakula bora, pia kinajishughulisha na uelimishaji Wananchi juu ya ugonjwa wa ukimwi.

``Sisi wenyewe ni mashahidi,tumejionea jinsi gani nguvu ya Taifa inavyopotea kutokana na nguvu kupungua hivyo basi sisi kama wataalamu wa afya tumeamua kusimama kidete katika kuwaelimisha Wananchi juu ya madhara yatokanayo na ugonjwa wa ukimwi ili nguvu kazi ya Taifa isipotee``anasema,Dkt Kefa.

Hata hivyo anasema kuwa elimu juu ya madhara yatokanayo na ukimwi wamekuwa wakiitoa kupitia warsha na makongamano mbalimbali Nchini,mashuleni na Vyuo vyote Nchini ili iwe rahisi kusambaa kwa wengine.

Anasema kuwa baada ya kituo hicho kutoa elimu ya madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwa wananchi wamekuwa na tabia yakuwatembelea Wananchi mara kwa mara ili kujua kama elimu kama imewafikia Wananchi.

``Tumekuwa na tabia ya kuwatembelea Wananchi wetu mara kwa mara ili kujua kama elimu imewafikia,nini kifanyike,wapi hawajaelewa ili wajiepushe na ugonjwa wa ukimwi.

Anaongeza kuwa kituo hicho pia ni sehemu moja wapo kwa Wananchi kujipatia ajira kutokana na kutoa elimu kwa wanaohitaji ili nao waanzishe vituo vyao.

Anasema kituo hicho kimeweza kutoa wataalamu mbalimbali kutokana na wengi wao kujua namna ya kupika, na kuandaa juisi mbalimbali kama juisi ya karoti ambayo wamekuwa wakiiuza ili wajipatie vipato vyao vya kila siku.

Dkt Kefa anasema kuwa kituo hicho kinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo vifaa vya kutolea huduma pamoja na uwezo wakuwalipia vipindi vitakavyowaelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kula vyakula bora,matunda,juisi ili waepukane na magonjwa ya mlipuko.

``Ninajitahidi elimu hii iwafikie Wananchi wangu kwa ukaribu na kwa urahisi,lakini ninaomba Serikali wadau na taasisi mbalimbali Nchini ziniunge mkono ili elimu hii iwafike kwa urahisi``anasema,Dr Kefa.

Anaomba Serikali wadau na taasisi mbalimbali Nchini zimuunge mkono kwakukisaidia kituo hicho fedha za kugharamia vipindi kwenye vyombo vya habari ili elimu hiyo ifike Tanzania nzima.

``Ninataka wakati sasa ufike hata Mwananchi aliyeko kijijini ajue juu ya umuhimu wa kula matunda ili wajiepushe na magonjwa nyemelezi katika miili yao,lakini yote haya yanawezekana kama tukipata fedha za kununu vipindi kwenye vyombo vyetu vya habari ili elimu hii iwafike Wananchi``anasema,Dkt Kefa.

No comments:

Post a Comment