Tuesday, June 12, 2012

HISTORIA YA FREEMASONS



HISTORIA YA KALE HADI FREEMASONS
Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza ni kwanini majina ya miungu wa kigiriki na wale wa Kirumi, ambao ustaarabu wao pia umechanulia mashariki ya kati ilikuwa ikiyatumia majina ya sayari kama majina ya miungu yao?
Walizijua vipi sayari hizo na majina yake enzi hizo za maelfu ya miaka kabla ya Masihi?. Nia yangu si kupatiwa majibu lakini kilicho kikubwa ni kwamba millennia nyingi wakati wa mpango  mkubwa wa kuichukua dunia ili iwe ya kabila fulani moja tu; 
Taarifa nyingi kuhusu historia ya kweli ya dunia zimekuwa zikifichwa na kupewa watu maalum kama ambavyo tutakavyoona huko mbele.
Kutufundisha kwamba binadamu wa kwanza alikuwa NYANI aliyeishi mamilioni ya miaka mingi huko nyuma na kwamba nyani huyo alianza kubadilika taratibu hadi akapatikana tunayemwita BINADAMU leo; hiyo yote ni sehemu ya kututupilia mbali na ukweli wa mambo.
Kwa maelfu ya miaka dunia imekuwa ikipitia mabadiliko na misukosuko kadhaa lakini hakuna hata moja lililopata kuelezewa na wale wanaoitwa WANAHISTORIA kwasababu si kazi yao.
Kazi yao ni kufundisha kile tu walichoambiwa na kuelekezwa wakifundishe. Masalio mengi ya kihistoria, yaliyopatikana miaka ya hivi karibuni ngesaidia kuibadili historia inayotumika hivi sasa. Kinachoshangaza yamewekwa kama mapambo kwenye majumba ya makumbusho.
Mfumo mzima wa elimu umeshikiliwa na KABILA HILO LA WAVAMIZI wanafahamu kipi kifundishwe kwenye Kemia , Baiolojia, Fizikia, Hisabati, Historia na fani nyingine mbalimbali.
Kwa miaka mingi sasa mfumo wa elimu umekuwa wa kukitukuza kile kilochofanywa na wasomi waliotangulia, wala hautoi nfasi kwa wasomi wa sasa nao kuwa wabunifu na hivyo kuleta maarifa mapya.
KWANINI?
Mtu kunakili kilichoandikwa kitabuni anaonekana kuwa na akili sana na mtu anayeelewa vyema somo.; Yule nayejaribu kuelezea kwa maneno yake ili kuonyesha ubunifu wake wa namna alivyolielewa somo husika nje ya mstari na nukta za vitabuni anaonekana hajui kitu kwa hiyo amekosea.
Huo ndio mfumo uliotengeneza tangu enzi na enzi ili kufanya binadamu awe mjinga maisha yake yote ili hali mkononi anacho cheti kinachomtambulisha kuwa ana shahada moja, mbili, tatu hata nne. Lakini kichwani mwake ni kama maktaba iliyojaa vitabu vilivyoandikwa na wengine.
Vitabu vyenye maneno na mawazo ya watu ambayo kwa miaka yote waliyokuwa shuleni walilazimishwa kuvikariri kama vilivyo na hakuna jipya waliloondoka nalao kwa kifupi hakuna lake hata moja! Je huyu kweli ni msomi au kabati la vitabu?.
MBINU kubwa waliyoitumia ana ambayo bado inatiliwa msisitizo kwa njia mbalimbali ni kuwafanya watu wa makabila mengine waendelee kuwa WAJINGA na WAPUMBAVU wa mwisho kabisa. Elimu na yale maarifa ya ukweli, wakayachukua wao.
KWA LEO NIISHIE HAPA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

No comments:

Post a Comment