IDARA YA HABARI NA WASEMAJI WA WIZARA, TAASISI NA HALMASHAURI ZA WILAYA NA MIKOA WATAKIWA KUJIPANGA KATIKA KUISEMEA SERIKALI

IDARA ya Habari (
MAELEZO) imetakiwa kujipanga vizuri ili kuweza kutekeleza majukumu yake
ya kuwa Msemaji wa Serikali ipasavyo; hatua hiyo itasaidia kuepusha
malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusiana na utendaji wa Serikali.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dkt. Fenella Mukangara wakati akifungua kikao kazi cha Maafisa Habari na
Mawasiliano wa Serikali katika ukumbi wa Victoria Palace Jijini Mwanza.
Aidha, Dkt. Mukangara
alisema, Idara ya Habari ( MAELEZO) ina jukumu zito la kuwa Msemaji
Mkuu wa Serikali . Hii ni kwa mujibu wa agizo la Serikali Na. C 16 la
mwaka 1977.
" Serikali inafanya
mambo mengi mazuri kwa wananchi lakini hayasemwi. Matokeo yake Serikali
inaishia kulaumiwa na wananchi bila sababu.
"Ndugu
zangu hali hii haikubaliki. Lazima tubadilike na lazima tuseme .
Hatuwezi kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali asiyesema." Alisema Dkt.
Mukangara.
Dkt. Mukangara
aliongeza kuwa Idara ya habari itekeleze jukumu hilo kwa kushirikiana na
Wasemaji wa Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali na Wasemaji hao
watambue kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ni Idara ya Habari.
Akizungumzia kuhusu
uhuru wa vyombo vya habari alisema,tunalo tatizo la baadhi ya vyombo vya
habari nchini kudhani kwamba uhuru wa vyombo vya habari hauna mipaka.
Hivyo alivitaka vyombo vya habari vitambue kuwa hakuna nchi yoyote
duniani ambayo utendaji wa vyombo vyake vya habri haubna mipaka.
" Wakati wote uhuru wa
vyombo vya habari popote pale huendana na wajibu hata ktika mataifa
yaliyoendelea"Alisema Dkt. Mukangara.
Aidha,
alivitaka vyombo vya habari kuwa makini katika kutangaza habari
zinazohusu mchakato wa mabadiliko ya katiba huku akisissitiza kuonyesha
uzalendo wa hali ya juu katika kuwahabarisha wananchi na kutoa elimu.
Dkt. Mukangara pia
aliwataka Maafisa hao kuhakikisha kwamba wanaelimisha wananchi juu ya
umuhimu wa zoezi la Sensa ya watu na Makazi.
Baadhi ya mada
zitakazojadiliwa katika kikao hicho cha siku tano chini ya Uenyekiti wa
Katibu
Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Sethi Kamuhanda, ni pamoja na Changamoto za
utaratibu wa usajili wa magazet; Changamoto zinazoikabili Tanzania
katika kuhama kutoka Analojia kwenda Digitali kufikia mwaka 2012;
Wajibu wa Maafisa Mawasiliano na mfumo wa mawasiliano Serikalini; na
Kazi za Serikali Mtandao na Tovuti kuu.
Kwa upande wake Afisa
Habari wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Bi Monica Mutoni alisema
kikao kazi hiki ni fursa kwa Maafisa Habari kuboresha kazi zao na
kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuwahabarisha wananchi majukumu ya
Serikali.
Naye Afisa Habari wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Bw. Leonidas Tibanga alisema kuwa baada ya kikao kazi hicho, Maafisa
Habari wataweza kupata ujuzi mpya kutokana na mada zitakazotolewa, na
kubadilishana uzoefu ikiwa ni pamoja na kuongeza wigo wa mawasiliano
miongoni mwao.
Vikao kazi vya Maafisa Habari vimekuwa vikifanyika kila mwaka chini
ya uratibu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamduni na Michezo ili
kujadili namna bora ya utoaji habari za Serikali na uimarishaji wa
mawasiliano kwa umma
No comments:
Post a Comment