HUYU NDIYE RAIS TUNAYE MUHITAJI DSJ
Usomi wa ngazi mbalimbali si sifa ya
mtu kufaa kuwa kiongozi, dunia katika historia yake ina majina lukuki ya baadhi
ya viongozi ambao walikuwa wasomi, lakini hatima ya uongozi wao haikutofautiana
na wajinga.
Hata hapa nchini kuna baadhi ya viongozi serikalini, kwenye mashirika na hata kwenye sekta binafsi ambao wakikuonesha vyeti vyao vya shule unaweza kuogopa, lakini utendaji wao ni kichefuchefu.
Kisaikolijia sifa za kiongozi ziko wazi na ni muhimu, mtu kuwa nazo kabla au baada ya kupewa cheo. Leo tunataka kuziangalia kwa undani sifa hizi, ili kama wananchi au viongozi wenye dhamana ya kuchagua watu wa kuongoza tuwatazame watu kwa sifa zao kabla na baada ya kuwapa nafasi. Sifa za kiongozi ni hizi zifuatazo:
Awaze mafanikio makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono ya juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake sekta yake inapata mafanikio makubwa, hii ndiyo itakuwa dira ya kazi yake itakayompa muongozo wa kusimamia wafanyakazi na watendaji wote walio chini yake kufikia kiwango cha mafanikio anachokiwaza. Kiongozi asiyekuwa na mawazo ya juu ya kuendelea kutoka mahali alipo hafai.
Awe na nia
Haitoshi kwa kiongozi kuwa na mawazo chanya peke yake bila kuwa na nia ya kuyatimiza. Hivyo, kiongozi atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo tu atakuwa na uwezo wa kuratibu vema na kutekeleza alichowaza. Ajue njia anayopita, awatangulie anaowaongoza kwa vitendo.
Ajitambue mwenyewe
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na upungufu wake na awe tayari kujiongezea maarifa kila siku, ili aweze kukabili changamoto na mabadiliko ya ulimwengu. Asome, afuatilie mambo yanavyokwenda na ajifunze kwa wenzake kuhusu kufanikisha malengo yake.
Asimamie maamuzi
Kuna wakati malengo hukumbana na vikwazo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kuwa mtu wa mwisho. Kiongozi mwenye kubadilika badilika kama kinyonga, hafai kwa vile kukosa msimamo kuna maanisha udhaifu wa mipango na kujiamini.
Adhibiti msongo wa mawazo
Tunamtarajia kiongozi mzuri awe ni mtu mwenye kupunguza msongo wa mawazo, ili kuifanya akili yake ifikie maamuzi sahihi, lakini kama atakuwa mwenye kuwaza mengi, atajikuta anachanganyikiwa na kuwa mtu wa jazba katika maamuzi na hivyo kuipotosha jamii.
Akubali kukosolewa
Viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia ya kuthibitisha msimamo wao na usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa kwa kutazama mwenendo wake na usahihi wake. Asiyekubali kukosolewa hafai kuwa kiongozi.
Awe msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasilikiza watu walio chini yake, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Lakini pia anatakiwa kuwafahamu kwa undani, ili aweze kuwaongoza vema kufuatana na hali zao. Akiwa na watu walemavu wenye kasoro kadhaa wa kadhaa anatakiwa kuwatambua kabla na baada ya kuwa kiongozi wao. Kuongoza usichokifahamu ni ujinga.
Afuate haki
Kiongozi imara anatakiwa kufuata haki katika kuongoza kwake, asijione mwenye haki zaidi ya wale anaowaongoza katika sheria. Ni muhimu kwake kuwafanya walio chini yake kujiona wako huru katika mawazo na matendo. Kiongozi anayetumia nguvu na ukali kuongoza watu hafai. Hata yule mwenye kujivunia uongozi wake naye hafai.
Awe egemeo la watu
Sifa nyingine ya kiongozi ni kuwa egemeo la watu wake katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza, kufurahi pamoja na watu wa chini yake bila kujitenga nao. Ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali na awe tayari kutumika zaidi kwa maslahi ya wengine.
Atie moyo watu
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuwatia moyo walio chini yake ili waweze kuendeleza vipaji vyao. Haipendezi kwa kiongozi kuwavunja moyo watu kwa kauli za kudharau kazi na jitihada zao walizojaribu kufanya katika kutekeleza majukumu yao kama wafanyakazi au wananchi.
Afurahie mafanikio
Sifa nyingine muhimu ya kiongozi ni kuwa tayari kufurahia mafanikio aliyopata pamoja na watu wake. Ni wajibu wa kiongozi kutoa tuzo, kuwashukuru wafanyakazi wake na kuwa tayari kuwapa ofa. Hii itasaidia kuwafanya watu waone hawajapoteza nguvu zao katika utendaji wao na kwamba wanakubalika. Si busara wakati mwingine kuwakosoa watu mbele ya hadhara na kueleza kutofurahishwa na kazi zao.
Aungane na wa chini yake
Mtu kuwa kiongozi haimaanishi amekuwa wa tofauti na watu wengine kiasi cha kushindwa kuchangamana nao kama wanavyofanya baadhi ya viongozi. Kiongozi mwema ni yule atakayeungana na watu wake katika maisha ya kawaida. Kuwa kiongozi haimaanishi kwamba watu watakufuata wewe kila siku, wakati mwingine wewe unatakiwa kuwafuata wao na kuwa nyuma yao hata mahali walipokosea au wanapokabiliwa na makosa, watetee na uoneshe kuwajali na kuwapigania, makosa utayahesabu baada ya utetezi wako kukamilika.
Akubali lawama
Kama kiongozi amefanya mambo ambayo jamii haikupendezwa nayo anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Ikiwa anaongoza kitego cha umeme kwa mfano na watu hawakupata nishati hiyo kwa wakati hatakiwi kukwepa lawama, vivyo hivyo kwenye wizara na idara au nchi kwa ujumla.
Afahamu kutatua matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo mzuri katika eneo hili umesimama katika mawasiliano na watu wa chini, mawasiliano haya ndiyo yatakayomuwezesha kiongozi kujua matatizo waliyonayo wafanyakazi wake au hata jamii anayoiongoza na hivyo kumfanya apate wasaa wa kuyashughulikia mapema.
Ajifunze kwa makosa
Wakati mwingine mawazo na mipango inaweza ikaenda kombo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kujifunza kutokana na makosa yake au ya wale anaowaongoza, ili kuepuka kurudia makosa yale yale na kumfanya apoteze sifa za kuwa kiongozi mzuri.
Mwanafalsafa Winston Churchill aliwahi kusema "The price of greatness is responsibility." Thamani ya ukuu ni uwajibikaji.
Awe mwaminifu
Miongoni mwa maeneo magumu kabisa yaliyowashinda na yanayoendelea kuwashinda viongozi wengi ni uaminifu. Kiongozi bora ni yule ambaye yuko tayari kusimamia muongozo wa katiba ya nchi au marufuku alizowekewa katika madaraka yake. Hii inakwenda sambamba na kutowaonea, kuwanyanyasa wa nchini yake kwa kutumia cheo chake.
Awe mkweli
Viongozi wengi hasa wa kisiasa siku hizi ni waongo hakuna mfano, wamejaa ahadi zisizotekelezeka na hata wanapogundua kuwa hawana uwezo au wamekwama kuzitimiza, hawaoni haja ya kutubu mbele ya wanaowaongoza. Kiongozi makini ni yule atayekuwa tayari kuonesha ubora wa matendo na kauli zake.
Asiwe mwenye majungu
Kuna baadhi ya viongozi kwenye maofisi wanaendekeza sana majungu na pengine kuyapa umuhimu wa hali ya juu. Hii ni sifa mbaya kwa kiongozi yo yote, hivyo anayetumikia ‘umbea’ katika ofisi aliyokabidhiwa kama mkuu anapaswa kuondolewa. Kiongozi makini atatumia uwezo wake kuzuia watu wasimsengenye/wasisengenyane kwa kuwa muwazi na mwenye kufungua milango ya watu kumuona na kumlaumu na kueleza hisia zao.
Awe bora
Kwa kila analofanya kama kiongozi lazima alifanye kwa ubora, asiwe mtu mwenye kulipua kazi na kufanya chini ya kiwango cha uwezo wake. Kila siku katika kazi, maamuzi, usimamizi, utekelezaji lazima atumike zaidi ya uwezo wake.
Hata hapa nchini kuna baadhi ya viongozi serikalini, kwenye mashirika na hata kwenye sekta binafsi ambao wakikuonesha vyeti vyao vya shule unaweza kuogopa, lakini utendaji wao ni kichefuchefu.
Kisaikolijia sifa za kiongozi ziko wazi na ni muhimu, mtu kuwa nazo kabla au baada ya kupewa cheo. Leo tunataka kuziangalia kwa undani sifa hizi, ili kama wananchi au viongozi wenye dhamana ya kuchagua watu wa kuongoza tuwatazame watu kwa sifa zao kabla na baada ya kuwapa nafasi. Sifa za kiongozi ni hizi zifuatazo:
Awaze mafanikio makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono ya juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake sekta yake inapata mafanikio makubwa, hii ndiyo itakuwa dira ya kazi yake itakayompa muongozo wa kusimamia wafanyakazi na watendaji wote walio chini yake kufikia kiwango cha mafanikio anachokiwaza. Kiongozi asiyekuwa na mawazo ya juu ya kuendelea kutoka mahali alipo hafai.
Awe na nia
Haitoshi kwa kiongozi kuwa na mawazo chanya peke yake bila kuwa na nia ya kuyatimiza. Hivyo, kiongozi atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo tu atakuwa na uwezo wa kuratibu vema na kutekeleza alichowaza. Ajue njia anayopita, awatangulie anaowaongoza kwa vitendo.
Ajitambue mwenyewe
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na upungufu wake na awe tayari kujiongezea maarifa kila siku, ili aweze kukabili changamoto na mabadiliko ya ulimwengu. Asome, afuatilie mambo yanavyokwenda na ajifunze kwa wenzake kuhusu kufanikisha malengo yake.
Asimamie maamuzi
Kuna wakati malengo hukumbana na vikwazo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kuwa mtu wa mwisho. Kiongozi mwenye kubadilika badilika kama kinyonga, hafai kwa vile kukosa msimamo kuna maanisha udhaifu wa mipango na kujiamini.
Adhibiti msongo wa mawazo
Tunamtarajia kiongozi mzuri awe ni mtu mwenye kupunguza msongo wa mawazo, ili kuifanya akili yake ifikie maamuzi sahihi, lakini kama atakuwa mwenye kuwaza mengi, atajikuta anachanganyikiwa na kuwa mtu wa jazba katika maamuzi na hivyo kuipotosha jamii.
Akubali kukosolewa
Viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia ya kuthibitisha msimamo wao na usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa kwa kutazama mwenendo wake na usahihi wake. Asiyekubali kukosolewa hafai kuwa kiongozi.
Awe msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasilikiza watu walio chini yake, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Lakini pia anatakiwa kuwafahamu kwa undani, ili aweze kuwaongoza vema kufuatana na hali zao. Akiwa na watu walemavu wenye kasoro kadhaa wa kadhaa anatakiwa kuwatambua kabla na baada ya kuwa kiongozi wao. Kuongoza usichokifahamu ni ujinga.
Afuate haki
Kiongozi imara anatakiwa kufuata haki katika kuongoza kwake, asijione mwenye haki zaidi ya wale anaowaongoza katika sheria. Ni muhimu kwake kuwafanya walio chini yake kujiona wako huru katika mawazo na matendo. Kiongozi anayetumia nguvu na ukali kuongoza watu hafai. Hata yule mwenye kujivunia uongozi wake naye hafai.
Awe egemeo la watu
Sifa nyingine ya kiongozi ni kuwa egemeo la watu wake katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza, kufurahi pamoja na watu wa chini yake bila kujitenga nao. Ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali na awe tayari kutumika zaidi kwa maslahi ya wengine.
Atie moyo watu
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuwatia moyo walio chini yake ili waweze kuendeleza vipaji vyao. Haipendezi kwa kiongozi kuwavunja moyo watu kwa kauli za kudharau kazi na jitihada zao walizojaribu kufanya katika kutekeleza majukumu yao kama wafanyakazi au wananchi.
Afurahie mafanikio
Sifa nyingine muhimu ya kiongozi ni kuwa tayari kufurahia mafanikio aliyopata pamoja na watu wake. Ni wajibu wa kiongozi kutoa tuzo, kuwashukuru wafanyakazi wake na kuwa tayari kuwapa ofa. Hii itasaidia kuwafanya watu waone hawajapoteza nguvu zao katika utendaji wao na kwamba wanakubalika. Si busara wakati mwingine kuwakosoa watu mbele ya hadhara na kueleza kutofurahishwa na kazi zao.
Aungane na wa chini yake
Mtu kuwa kiongozi haimaanishi amekuwa wa tofauti na watu wengine kiasi cha kushindwa kuchangamana nao kama wanavyofanya baadhi ya viongozi. Kiongozi mwema ni yule atakayeungana na watu wake katika maisha ya kawaida. Kuwa kiongozi haimaanishi kwamba watu watakufuata wewe kila siku, wakati mwingine wewe unatakiwa kuwafuata wao na kuwa nyuma yao hata mahali walipokosea au wanapokabiliwa na makosa, watetee na uoneshe kuwajali na kuwapigania, makosa utayahesabu baada ya utetezi wako kukamilika.
Akubali lawama
Kama kiongozi amefanya mambo ambayo jamii haikupendezwa nayo anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Ikiwa anaongoza kitego cha umeme kwa mfano na watu hawakupata nishati hiyo kwa wakati hatakiwi kukwepa lawama, vivyo hivyo kwenye wizara na idara au nchi kwa ujumla.
Afahamu kutatua matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo mzuri katika eneo hili umesimama katika mawasiliano na watu wa chini, mawasiliano haya ndiyo yatakayomuwezesha kiongozi kujua matatizo waliyonayo wafanyakazi wake au hata jamii anayoiongoza na hivyo kumfanya apate wasaa wa kuyashughulikia mapema.
Ajifunze kwa makosa
Wakati mwingine mawazo na mipango inaweza ikaenda kombo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kujifunza kutokana na makosa yake au ya wale anaowaongoza, ili kuepuka kurudia makosa yale yale na kumfanya apoteze sifa za kuwa kiongozi mzuri.
Mwanafalsafa Winston Churchill aliwahi kusema "The price of greatness is responsibility." Thamani ya ukuu ni uwajibikaji.
Awe mwaminifu
Miongoni mwa maeneo magumu kabisa yaliyowashinda na yanayoendelea kuwashinda viongozi wengi ni uaminifu. Kiongozi bora ni yule ambaye yuko tayari kusimamia muongozo wa katiba ya nchi au marufuku alizowekewa katika madaraka yake. Hii inakwenda sambamba na kutowaonea, kuwanyanyasa wa nchini yake kwa kutumia cheo chake.
Awe mkweli
Viongozi wengi hasa wa kisiasa siku hizi ni waongo hakuna mfano, wamejaa ahadi zisizotekelezeka na hata wanapogundua kuwa hawana uwezo au wamekwama kuzitimiza, hawaoni haja ya kutubu mbele ya wanaowaongoza. Kiongozi makini ni yule atayekuwa tayari kuonesha ubora wa matendo na kauli zake.
Asiwe mwenye majungu
Kuna baadhi ya viongozi kwenye maofisi wanaendekeza sana majungu na pengine kuyapa umuhimu wa hali ya juu. Hii ni sifa mbaya kwa kiongozi yo yote, hivyo anayetumikia ‘umbea’ katika ofisi aliyokabidhiwa kama mkuu anapaswa kuondolewa. Kiongozi makini atatumia uwezo wake kuzuia watu wasimsengenye/wasisengenyane kwa kuwa muwazi na mwenye kufungua milango ya watu kumuona na kumlaumu na kueleza hisia zao.
Awe bora
Kwa kila analofanya kama kiongozi lazima alifanye kwa ubora, asiwe mtu mwenye kulipua kazi na kufanya chini ya kiwango cha uwezo wake. Kila siku katika kazi, maamuzi, usimamizi, utekelezaji lazima atumike zaidi ya uwezo wake.
Nguzo imara ya mwanafunzi yeyote anayetaka kufanikiwa katika
masomo yake ni kuwa mfuasi wa UTII na UAMINIFU mahali popote na kwa mtu yeyote.
Nakumbuka wakati nikiwa shule ya sekondari nilikiuka sana mambo haya muhimu,
nilikuwa mtu wa vurugu na mwanzilishi wa migomo.
Wakati huo sikuona kama nilikuwa nafanya makosa, mara zote nilijitazama kama shujaa kwa vile jamii, walimu na wanafunzi wenzangu walikuwa wakiniogopa. Kifupi nilikuwa na akili darasani lakini matokeo ya mwisho yalipotoka yalinishangaza kwani nilifeli.
Kushindwa huko kulinirudisha kwenye mikono ya wazazi ambao tayari nao nilikuwa nimewachosha kwa tabia zangu. Toka hapo hakuna mjomba wala shangazi aliyejitokeza kunisaidia kimasomo kwa kuwa sikuwa mtu wa kuaminiwa. Nilikaa nyumbani kama mtu muhuni kwa miaka mitano hadi nilipokubali kubadili tabia yangu.
Nilifikia uamuzi huo kwa sababu nilinusurika kufungwa jela baada ya kushiriki katika ugomvi ulioleta harufu ya mauaji ya kijana mmoja tuliyekuwa tukigombana naye. Nililazimika kutoroka na kukaa uhamishoni kwa miaka kadhaa. Baadaye nilikutana na maisha magumu ambayo siwezi kuyasahau.
Nakumbuka wakati huo wa dhiki nilijutia utundu nilioufanya shule kwa kuchezea elimu na kujikita katika mambo ya kihuni ambayo hayakunisaidia. Mwezi wa nane mwaka 1998 nilikubali kubadilika na kuanza kujifunza upya maisha ya utii na uaminifu chini ya uongozi wa walimu wa dini yangu ya kikristo.
Mafundisho ya kidini yalinisaidia kuacha ulevi na uvutaji wa sigara. Marekebisho hayo ya tabia yalinijenga zaidi upande wa rafiki zangu niliokuwa nasali nao, lakini ndugu walikuwa bado wananitilia shaka. Rafiki zangu hawakupata shida tena kunituma kusimamia ujenzi wa nyumba zao na miradi yao na mara nyingine niligeuka kuwa ‘benki’ nikawa natunza pesa za watu.
Simulizi ni ndefu lakini mwisho wa yote uaminifu wangu huo ndiyo uliomsukuma mmoja kati ya rafiki zangu kujitolea kunisomesha masomo ya jioni ili nirudie masomo niliyofeli nilipopata nafasi hiyo sikuichezea kwani tayari nilikuwa nimeonja machungu ya ujinga. Nilijituma kusoma kwa malengo na kufanikiwa kusahihisha cheti changu.
Nilipomaliza nilichagua fani ya uandishi wa habari, ambapo alitokea mama mmoja niliyemheshimu na kumtii akanisaidia tena kunisomesha. Kifupi maisha yangu yalikuwa ya kubebwa na watu niliowaonesha uaminifu na utii wangu.
Hawa ni rafiki zangu wa hapa nchini achilia mbali Dr ………………… kutoka chuo cha American Psychology ambaye alijitolea kunifundisha masomo ya Saikolojia elimu ambayo ilinifumbua macho na kuniwezesha kuwa hivi nilivyo sasa.
Huu ni ushuhuda wangu kwa ufupi, ambao nimeutoa kwa lengo la kuwafundisha kwa vitendo nguvu ya uaminifu na utii katika maisha ya kila siku ya mwanadamu na hasa kwa wanafunzi ambao safari ya kupata elimu inahitaji ushirikiano wa watu wanaoishi nao nyumbani na shuleni.
Wanafunzi wengi wameshindwa kufanikiwa kwa sababu ya kutokuwa waaminifu na watii kama nilivyoeleza huko nyuma, jambo ambalo limewafanya watengwe na jamii mithili ya yale yaliyonitokea mimi.
Ifahamike kuwa mwanafunzi hawezi kupata msaada wa kutosha kwa wazazi, walimu na ndugu zake kama atakuwa akipewa ada anaitumia vibaya, akiwa na kashfa za ngono, wizi, uvutaji bangi na utumiaji wa dawa za kulevya na kuonesha ukorofi.
MADA HII INAENDELEA UNAWEZA KUIPATA KWA KIREFU KAMA UTANUNU KITAMBU CHANGU CHA SAIKOLOJIA MBINU 100 ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI. KINAUZWA NA WAUZA MAGEZETI NCHI NZIMA
Wakati huo sikuona kama nilikuwa nafanya makosa, mara zote nilijitazama kama shujaa kwa vile jamii, walimu na wanafunzi wenzangu walikuwa wakiniogopa. Kifupi nilikuwa na akili darasani lakini matokeo ya mwisho yalipotoka yalinishangaza kwani nilifeli.
Kushindwa huko kulinirudisha kwenye mikono ya wazazi ambao tayari nao nilikuwa nimewachosha kwa tabia zangu. Toka hapo hakuna mjomba wala shangazi aliyejitokeza kunisaidia kimasomo kwa kuwa sikuwa mtu wa kuaminiwa. Nilikaa nyumbani kama mtu muhuni kwa miaka mitano hadi nilipokubali kubadili tabia yangu.
Nilifikia uamuzi huo kwa sababu nilinusurika kufungwa jela baada ya kushiriki katika ugomvi ulioleta harufu ya mauaji ya kijana mmoja tuliyekuwa tukigombana naye. Nililazimika kutoroka na kukaa uhamishoni kwa miaka kadhaa. Baadaye nilikutana na maisha magumu ambayo siwezi kuyasahau.
Nakumbuka wakati huo wa dhiki nilijutia utundu nilioufanya shule kwa kuchezea elimu na kujikita katika mambo ya kihuni ambayo hayakunisaidia. Mwezi wa nane mwaka 1998 nilikubali kubadilika na kuanza kujifunza upya maisha ya utii na uaminifu chini ya uongozi wa walimu wa dini yangu ya kikristo.
Mafundisho ya kidini yalinisaidia kuacha ulevi na uvutaji wa sigara. Marekebisho hayo ya tabia yalinijenga zaidi upande wa rafiki zangu niliokuwa nasali nao, lakini ndugu walikuwa bado wananitilia shaka. Rafiki zangu hawakupata shida tena kunituma kusimamia ujenzi wa nyumba zao na miradi yao na mara nyingine niligeuka kuwa ‘benki’ nikawa natunza pesa za watu.
Simulizi ni ndefu lakini mwisho wa yote uaminifu wangu huo ndiyo uliomsukuma mmoja kati ya rafiki zangu kujitolea kunisomesha masomo ya jioni ili nirudie masomo niliyofeli nilipopata nafasi hiyo sikuichezea kwani tayari nilikuwa nimeonja machungu ya ujinga. Nilijituma kusoma kwa malengo na kufanikiwa kusahihisha cheti changu.
Nilipomaliza nilichagua fani ya uandishi wa habari, ambapo alitokea mama mmoja niliyemheshimu na kumtii akanisaidia tena kunisomesha. Kifupi maisha yangu yalikuwa ya kubebwa na watu niliowaonesha uaminifu na utii wangu.
Hawa ni rafiki zangu wa hapa nchini achilia mbali Dr ………………… kutoka chuo cha American Psychology ambaye alijitolea kunifundisha masomo ya Saikolojia elimu ambayo ilinifumbua macho na kuniwezesha kuwa hivi nilivyo sasa.
Huu ni ushuhuda wangu kwa ufupi, ambao nimeutoa kwa lengo la kuwafundisha kwa vitendo nguvu ya uaminifu na utii katika maisha ya kila siku ya mwanadamu na hasa kwa wanafunzi ambao safari ya kupata elimu inahitaji ushirikiano wa watu wanaoishi nao nyumbani na shuleni.
Wanafunzi wengi wameshindwa kufanikiwa kwa sababu ya kutokuwa waaminifu na watii kama nilivyoeleza huko nyuma, jambo ambalo limewafanya watengwe na jamii mithili ya yale yaliyonitokea mimi.
Ifahamike kuwa mwanafunzi hawezi kupata msaada wa kutosha kwa wazazi, walimu na ndugu zake kama atakuwa akipewa ada anaitumia vibaya, akiwa na kashfa za ngono, wizi, uvutaji bangi na utumiaji wa dawa za kulevya na kuonesha ukorofi.
MADA HII INAENDELEA UNAWEZA KUIPATA KWA KIREFU KAMA UTANUNU KITAMBU CHANGU CHA SAIKOLOJIA MBINU 100 ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI. KINAUZWA NA WAUZA MAGEZETI NCHI NZIMA
DALILI KUMI NA TATU
ZA MIMBA
MWANAMKE anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida. Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.
“Homoni zinazosambaa mwilini mara tu unapopata ujauzito husababisha mabadiliko kadhaa katika mwili wake ambayo yanaweza kugundulika kabla hata ya uchunguzi halisi wa kujua kama mjauzito au la,” anasema Melissa Goist, Profesa na Mtalaama wa Masuala ya Uzazi wa Chuo Kikuu cha Ohio, Marekani.
Maumivu kwenye matiti
Hii ni dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati yai linavyopata “rutuba”, jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.
Maumivu mwilini
Utaanza kusikia maumivu kama vile unataka kuingia katika siku zako. Kwa kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha maumivu hayo.
Kutokwa damu bila kutegemea
"Wanawake wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao. Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25 ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai,” anasema Goist. Ambaye anaendelea kusema kwamba iwapo utaona hedhi yako inakuwa fupi au inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, unashauriwa kwenda kufanya kipimo cha ujauzito..
Kuchoka
Unapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati ukiwa kazini, lazima ufahamu kwamba mwili wako unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha mabadiliko.
“Tambua kwamba katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza kutumia sehemu ya nguvu zako na hivyo kukuletea uchovu na usingizi” anasema Goist.
Chuchu kuwa nyeusi
Chuchu huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza kufanya kazi kwa nguvu zaidi. Hata hivyo, Goist anasema: “Wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite.”
Kichefuchefu
Hali hii huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa na ujauzito, ambapo nyakati za asubuhi ndipo hasa hujionyesha.
Mwili kuvimba
Kuna wakati kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kukusababishia kuona tumbo limevimba na nguo zikawa zinakubana kutokana na chakula kujaa katika utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema ukatambua kwamba tayari una ujauzito na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.
Kwenda haja ndogo mara kwa mara
Kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu chako kimeanza kufanya kazi ya ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa ujauzito. Hali hii pia hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.
Tamaa ya vitu mbalimbali
Kutokana na mwili kuwa na “mzigo” wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili wake. Hii ni pamoja na kutaka vyakula fulani au kufanya mambo ambayo hapo nyuma alikuwa hayapendi.
Kuumwa kichwa
Kuongezeka kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususani katika wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.
Kufunga choo
Homoni ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo hali hii inaweza kujitokeza zaidi wakati ujauzito unapoendelea kukua.
Kuwa na hasira
"Kutokana na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia uchovu, na kukufanya kuwa na hasira,” anasema Goist
Kuongezeka kwa joto mwilini
Kipimo cha joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna “mtoto anakuja”.
No comments:
Post a Comment